logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Najuta sana kumuumiza mke wangu ambaye ni yatima

Wekesa alisema anajuta sana kumtusi mzazi huyo mwenzake hasa kwa kuwa yeye ni yatima.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho22 April 2025 - 08:57

Muhtasari


  • Wekesa alisema ndoa yake ya miaka miwili ilivunjika mwaka wa 2022 wakati ambapo alikosana na mkewe kwa kumtusi alipoomba pesa.
  • "Ningependa anisamehe ikiwezekana turudiane. Kama amepata mwingine ni sawa,” alisema.

Watangazaji Gidi na Ghost

Michael Wekesa mwenye umri wa miaka 41 kutoka Bungoma alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na aliyekuwa mke wake Sabina Mwikali (28) ambaye alikosana naye takriban miaka mitatu iliyopita.

Wekesa alisema ndoa yake ya miaka miwili ilivunjika mwaka wa 2022 wakati ambapo alikosana na mkewe kwa kumtusi alipoomba pesa.

“Nilikuwa nakaa na Mwikali Machakos. Tulipatana tukaelewana tukaanza kukaa na yeye. Ikafika mahali akataka kurudi chuo. Alipoenda chuo na mimi nikarudi kwetu Bungoma. Nikiwa Bungoma akaniomba pesa za mahitaji,” Wekesa alisema.

“Wakati huo sikuwa na kazi. Aliomba shilingi elfu mbili kila mwezi. Nikamwambia sina kazi. Yeye akasisitiza nikakasirika na yeye nilimuuliza “kwani anafikiria pesa nachota kwa mchanga”,” aliongeza.

Wekesa alisema anajuta sana kumtusi mama huyo wa mtoto wake mmoja hasa kwa kuwa yeye ni yatima.

“Tuliongea mara ya mwisho kama miezi saba imepita. Ningependa anisamehe ikiwezekana turudiane. Kama amepata mwingine ni sawa,” alisema.

Kwa bahati mbaya, Patanisho hiyo iligonga mwamba kwani kulitokea matatizo ya mawasiliano.

Je, una maoni ama ushauri gani kuhusu Patanisho ya leo?


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved