logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Nilifungua duka kutumia mkopo, nikaingia aviator iniletee pesa nijiboost, ikanikula - Jamaa asimulia ndoa ilivyovunjika

Okello alikiri kwamba mkewe alishughulikia mahitaji hadi Februari mwaka huu ambapo alichoka naye na kumfukuza.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho23 April 2025 - 09:23

Muhtasari


  • Okello alisema ndoa yake ya miaka mitatu ilisambaratika Februari wakati mkewe alimfukuza kwa kutoshughulikia mahitaji ya nyumbani.
  • “Mimi sijui kama amewadanganya. Mimi simjui,” alisema Irene kisha akakata simu.

Ghost na Gidi

Stanlus Okello mwenye umri wa miaka 28 kutoka Mbita, Homa Bay County alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mke wake Irene Akoth (28) ambaye alikosana naye mapema mwaka huu.

Okello alisema ndoa yake ya miaka mitatu ilisambaratika Februari mwaka huu wakati ambapo mkewe alimfukuza kwa nyumba kwa kutoshughulikia mahitaji ya boma.

Alisema kwamba masaibu yake ya kifedha yalianza mwaka jana wakati ambapo alichukua mikopo, na pia kujitosa katika mchezo wa Kamari.

“Tulikuwa tunaishi pamoja alafu nilikuwa na mashida. Nilichukua mkopo, dadangu akawa na emergency akaomba Sh250k. Nikachukua mkopo mwingine. Sasa pesa ikawa kidogo kwa sababu nilikuwa nakatwa pesa,” Okello alisimulia.

“Kuanzia Septemba nikalemewa kwa sababu duka nilikuwa nimefungua kutumia mkopo nilienda nikaingia mchezo ya aviator nione kama inaweza ikaleta pesa kidogo nijiboost nayo. Ikanikula vile. Kuanzia hiyo Septemba sikuwa na kitu nikaacha kushughulikia mahitaji. Nikipata kitu kidogo pia wazazi walikuwa wananitegemea juu mimi ndiye firstborn,” aliongeza.

Okello alikiri kwamba mkewe alisaidia kwa mahitaji muhimu ya nyumbani kwa miezi kadhaa hadi Februari mwaka huu ambapo alichoka naye na kumfukuza.

“Mpaka Februari, mke wangu alikuwa ananishikilia mambo kama kodi. Kufikia Februari mke akaniambia hatuwezi endelea hivyo itabidi nimeenda nyumbani nijifikirie. Sikuongea sana nikakubali nikatoka,” alisema.

“Hivi majuzi nimetamani kumuongelesha lakini ameniblock. Aliniambia hataki mambo yangu, nashindwa itakuwaje na tuko na watoto wawili. Saai niko sawa. Sijamaliza kulipa mkopo lakini mambo iko sawa. Sijawahi kumkosea kwa njia nyingine,” aliongeza.

Irene alipopigiwa simu, kwa mshangao alimruka Okello.

“Mimi sijui kama amewadanganya. Mimi simjui,” alisema Irene kisha akakata simu.

Okello alisema, “Ananijua. Itabidi nianze upya.”

"Kulikuwa na stori nyingine ya relatives. Wajomba zangu na mama yangu hawakuwa wanampenda. Walikuwa wanaona kama ni mtu mbaya lakini mimi sikuwa naona ubaya wake,” alisema.

Aliongeza kwamba hakuna haja ya kumtafuta tena mama huyo wa watoto wake wawili na kueleza kuwa Patanisho ilikuwa tegemeo lake la mwisho kurejesha ndoa yake.

“Achana nayo. Nilidhani nitajaribu ya mwisho na nyinyi. Haina haja nimbembeleze sana. Akiamua kurudi ni sawa… Namtakia maisha mema. Kama kuna kitu anahitaji usaidizi kwa watoto asiogope kunipigia simu,” alisema.

Je, una maoni ama ushauri gani kuhusu Patanisho ya leo?

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved