logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hamisa Mobetto Alilipiwa Mahari Ya Ng’ombe 150 Wala Sio 30 – Mamake Athibitisha

Mamake Hamisa Mobetto alisema kwamba ng’ombe ambao mchezaji huyo alitoa kama mahari ni 150 pamoja na kiasi cha pesa nyingi.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 February 2025 - 15:15

Muhtasari


  • “Nadhani ilikuwa mubashara jamani kila mtu ameona ng’ombe wale wamesimama. Ng’ombe walikuwa nadhani malori mawili na walienda kwa mamangu.”
  • Mama huyo alisema kwamba yeye ametoka katika familia ya chifu na kwao ni sheria mahari kulipwa kwa kutumia ng’ombe walio hai.
  • “Kwa hiyo wao walileta ng’ombe 150 na kiasi cha pesa ambacho siwezi kukitaja,” mama mtu alisisitiza.

Mamake Hamisa Mobetto amethibitisha mwanasoka Aziz Ki alilipa mahari ya ng'ombe 150

NI Rasmi sasa kwamba mwanamitindo Hamisa Mobetto na mwanasoka Stephane Aziz Ki ni mtu na mkewe baada ya wawili hao kukamilisha taratibu zote za ndoa.

Mwanamitindo huyo, mama wa watoto wawili alifunga harusi na Stephane Aziz Ki, mchezaji wa Klabu ya Yanga nchini Tanzania ambaye ni raia wa Burkina Faso, Afrika Magharibi.

Aziz Ki alilipa mahari na sasa mamake Mobetto asmefichua idadi ya ng’ombe ambao mchezaji huyo alitoa.

Akizungumza na Zamaradi TV katika mahojiano ya baada ya shughuli, mamake Hamisa Mobetto alisema kwamba ng’ombe ambao mchezaji huyo alitoa kama mahari ni 150 pamoja na kiasi cha pesa nyingi.

Mama mtu alisisitiza kwamba ng’ombe hawakuwa 30 kama ambavyo baadhi ya watu walijaribu kusema mitandaoni, akisema kuwa malori yaliyokuwa yamebeba ng’ombe hao yalipiga foleni hadi nyumbani kwake.

“Nadhani ilikuwa mubashara jamani kila mtu ameona ng’ombe wale wamesimama. Ng’ombe walikuwa nadhani malori mawili na walienda kwa mamangu.”

“Sijawahesabu kwa sababu unajua nilikuwa kwenye furaha na mihemko lakini ng’ombe tuliokubaliana nao ni 100. Unajua ng’ombe mmoja mzima ni shilingi milioni 3.5. lakini wao walileta ng’ombe kama 150, wengine walipelekwa kwa mama, wale walioonekana pale ni wachache,’ alisema.

Mama huyo alisema kwamba yeye ametoka katika familia ya chifu na kwao ni sheria mahari kulipwa kwa kutumia ng’ombe walio hai.

“Kwa hiyo wao walileta ng’ombe 150 na kiasi cha pesa ambacho siwezi kukitaja,” mama mtu alisisitiza.

Awali, kulikuwa na taarifa kwamba Aziz Ki alilipa jumla ya ng’ombe 30.

Wakati wa hafla hiyo, Hamisa Mobetto alisema anamshukuru Mungu kwa kumpa mpenzi anayemuona kuwa ndiye sahihi kwake na sasa rasmi ni mchumba wa mtu anayempenda kwa dhati.

 "Sasa hapa ndipo nimefika, kwa kuwa nimekutana na mtu mwenye mapenzi ya kweli kwangu. Pia, nafsi zetu zimeendana. Namuomba Mungu anyooshe mambo yaende kama tulivyopanga,"  Hamisa aliambia Mwanaspoti.

 Naye Aziz Ki alisema anaamini safari yake ya muda mrefu ya kutafuta mke imefikia mwisho, kwani amempata mwanamke anayempenda kutoka ndani ya moyo wake.

 "Taratibu zote za uchumba nimekamilisha. Kilichobaki sasa ni ndoa tu, ambayo itafungwa kesho, Jumapili, Februari 16, 2025. Sherehe rasmi inatarajiwa kufanyika Februari 19, 2025, katika ukumbi wa The SuperDome, Masaki, jijini Dar es Salaam," alisema Aziz Ki.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved