logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mike Sonko Ataja Sababu Ya Kuwapa Watu Zawadi Za Kondomu Siku Ya Wapendanao

Sonko ambaye alikuwa ameandamana na timu yake jijini Nairobi alisambaza zawadi za mandhari ya Valentino zikiwemo maua, divai na vitu vingine vya kuonyesha mapenzi.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 February 2025 - 08:52

Muhtasari


  • USAID ilitangaza kusitisha shughuli zake katika mataifa kadhaa duniani baada ya rais mpya wa Marekani, Donald Trump kuagiza kukatwa kwa misaada 

Mike Sonko akisambaza mipira ya kondomu siku ya valentine's day

MWISHONI mwa juma lililopita, Wakenya wa matabaka mbalimbali waliungana na ulimwengu kusherehekea siku ya wapendanao kwa kutunukiana zawadi mbalimbali.

Aliyekuwa gavana wa Nairobi, Mike Sonko ni mmoja wa watu maarufu waliojitokeza kusherehekea siku hiyo kwa njia tofauti ambapo aliamua kusambaza zawadi kwa watu mitaani.

Sonko ambaye alikuwa ameandamana na timu yake jijini Nairobi alisambaza zawadi za mandhari ya Valentino zikiwemo maua, divai na vitu vingine vya kuonyesha mapenzi.

Mhisani huyo aliwashangaza wengi alipoamua pia kujumuisha mipira ya kushiriki mapenzi katika zawadi zake na kuwapa watu, zawadi ambazo zilipata mapokezi ya kipekee.

Sonko alipeleka kwenye ukurasa wake wa X akaeleza sababu ya kusambaza zawadi za aina hiyo, akisema kwamba aliona ni vyema kuwapa watu mipira ya kujikinga dhidi ya maradhi ya zinaa kwa sababu shirika la Marekani, USAID ambalo kwa muda mrefu limekuwa likisambaza kondomu kwa watu limesitisha shughuli zake.

“Tunapoadhimisha Siku ya Wapendanao leo, nilisambaza zawadi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na maua, chokoleti, mvinyo, na hata kondomu za ladha kwa ajili ya kujilinda, kutokana na kwamba USaid haipo nasi tena na imeondoa msaada wake,” Sonko alisema.

USAID ilitangaza kusitisha shughuli zake katika mataifa kadhaa duniani baada ya rais mpya wa Marekani, Donald Trump kuagiza kukatwa kwa misaada kwa mataifa ya nje, katika sera yake ya ‘Marekani Kwanza’.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved