logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Abba Marcus: Mwanawe Jose Chameleone Amuita ‘Baba Mbaya Zaidi Katika Historia’

Kupitia ukurasa wa X, Marcus alifoka vikali alimlaani babake na kumuita ‘Baba mbaya zaidi kuwahi kutokea katika historia ya dunia’

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani20 February 2025 - 09:56

Muhtasari


  • "I have the one of the one of the worse father in the history of the world 😂" alichapisha, kabla ya kushiriki machapisho kadhaa akielezea kufadhaika kwake.
  • Hii si mara ya kwanza kwa Marcus kumkosoa babake hadharani.

Abba Marcus na babake Jose Chameleone

ABBA Marcus, mwanawe msanii nguli wa muda mrefu kutoka Uganda, Jose Chameleone ameibuka tena na mashambulizi makali dhidi ya babake, saa chache baada ya taarifa za msanii huyo kutakiwa kufanyiwa matibabu ya kina kuibuka.


Kupitia ukurasa wa X, Marcus alifoka vikali alimlaani babake na kumuita ‘Baba mbaya zaidi kuwahi kutokea katika historia ya dunia’ wakati ambapo Chameleone anaelekea kufanyiwa upasuaji wa kongosho.


"I have the one of the one of the worse father in the history of the world 😂" alichapisha, kabla ya kushiriki machapisho kadhaa akielezea kufadhaika kwake.


Hii si mara ya kwanza kwa Marcus kumkosoa babake hadharani.


Matamshi yake ya hivi punde yanaonekana kutokana na kisa cha hivi majuzi ambapo Chameleone alikimbizwa hospitalini lakini akachagua kuzungumzia uvumi wa uongo kumhusu kwenye video ya moja kwa moja ya TikTok kabla ya kuzungumza na watoto wake.


"Chameleone a ho... alikimbizwa hospitalini na jambo la kwanza analofanya badala ya kuwasiliana na watoto wake, anaendesha TikTok live lol 😂😂😂" alichapisha Marcus, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Chameleone na Daniella Atim.


Kijana huyo amekuwa akimshambulia babake mara kwa mara kwenye mitandao ya kijamii, zaidi ya miezi miwili sasa tangu alipolazwa.


“Sifanyi hivi ili kufichua hulka za huyo mtu, ningeweza kuzembea kuanika hovyo hovyo. Yeyote mwenye akili anajua yeye ni nani. Niko kwenye jukwaa LANGU nikijieleza kwa sababu mtandao wa kijamii ni wa kujieleza,’ alijitetea katika moja ya machapisho yake.


 


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved