logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Hujui Chochote Kuhusu Uhusiano Wangu Na Babako!” Mkewe Besigye Ajibu Mwanawe Museveni

Winnie alimuonya Muhoozi zaidi akisema kwamba ikiwa ataendelea kuzungumzia uhusiano wake wa zamani na Museveni basi itambidi atoe ukweli mgumu ambao utamchanganya na kumfanya kujuta.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani23 February 2025 - 14:17

Muhtasari


  • Jenerali Kainerugaba, ambaye ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, alienda kwa X kusimulia jinsi uhusiano kati ya Museveni na Byanyima ulivyomalizika.
  • Muhoozi alitoa tamko lake saa chache baada ya Winnie kudai kwamba katika kitabu chake kijacho, atasimulia kwa sehemu kuhusu uhusiano wake wa zamani na Museveni kabla ya kuachana na kuoana na Besigye.

Gen Muhoozi Kainerugaba, Winnie Byanyima

WINNIE Byanyima, mke wa mwanasiasa wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye na ambaye anatajwa kuwa mpenzi wa zamani war ais Yoweri Museveni amemuonya mwanawe rais huyo, Muhoozi Kainerugaba dhidi ya kuzungumzia uhusiano huo wa zamani, akisema hajui chochote.


Kupitia ukurasa wake wa X, Byanyima alimuonya Muhoozi dhidi ya kukurupukia na kupayukia suala la uhusiano wake wa zamani na Museveni, akisema kwamba ni uhusiano uliokuwa changamano zaidi na ambao wote – yeye na Museveni, waliamua kuutupa katika kaburi la sahau na kila mmoja kujishughulisha na ya kwake.


"@mkainerugaba IWE MWANA WE…. Yetwaare. Ninahisi ni muhimu kuwa wazi: Kuna historia ngumu zaidi kati ya baba yako na mimi ambayo sote tumechagua kuvuka kwa kuheshimiana," Byanyima alichapisha kwenye X.


Winnie alimuonya Muhoozi zaidi akisema kwamba ikiwa ataendelea kuzungumzia uhusiano wake wa zamani na Museveni basi itambidi atoe ukweli mgumu ambao utamchanganya na kumfanya kujuta.


"Hata hivyo, ikiwa utaendelea kuwasilisha simulizi ya uwongo, huenda nikahitaji kutoa ushahidi MGUMU wa ukweli. Napendelea kudumisha mtazamo wetu wenye heshima, lakini chaguo hilo linabaki kuwa lako. Ninaona kuwa suala hili limefungwa."


Jenerali Kainerugaba, ambaye ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, alienda kwa X kusimulia jinsi uhusiano kati ya Museveni na Byanyima ulivyomalizika.


Muhoozi alitoa tamko lake saa chache baada ya Winnie kudai kwamba katika kitabu chake kijacho, atasimulia kwa sehemu kuhusu uhusiano wake wa zamani na Museveni kabla ya kuachana na kuoana na Besigye.


"HAKUNA kitu cha kawaida katika uhusiano wako na baba yangu. Ulipata nyumba yenye furaha ukajaribu kuibomoa. Wewe ni MSIBA wa mwanamke!! Hukutoka. Mzee alikufukuza nyumbani Desemba 1986, akakuburuza hadi kwenye gari huku unalia na kukupeleka kwa wazazi wako."


Kabla ya kufunga ndoa na Dk Kizza Besigye Julai 7, 1999, huko Nsambya, Kampala, Byanyima alikuwa akihusishwa kimapenzi na Museveni. Yeye na Besigye wana mtoto wa kiume, Anselm Besigye, ambaye kwa sasa anafuata PhD katika Chuo Kikuu cha Columbia huko New York.


 


 


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved