logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hata kama sina mke lakini niko na House-boy anayenadhifisha nyumba yangu – Salasya

“Mwanamuziki alishangaa kupata nyumba iliyopangwa vizuri isiyo na mke hehe ingawa nilimpa changamoto niko na house boy anafanya kazi ya ajabu,” Salasya alieleza.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 March 2025 - 10:30

Muhtasari


  • Alisema kwamba kijana huyo alipata changamoto kuona nyumbani kwake ni safi na nadhifu licha ya mbunge huyo kutokuwa na mke.
  • Hata hivyo, Salasya alifichua kwamba ako na kijana wa kiume ambaye anamsaidia katika usafi wa nyumba yake.

Peter Salasya, mbunge wa Mumias Mashariki

MBUNGE wa Mumias Mashariki. Peter Salasya ameweka wazi kwamba mazingira ya nyumbani kwake katika kaunti ya Kakamega ni safi licha ya kutokuwa na mke.

Mbunge huyo mcheshi ambaye katika siku za hivi karibuni amekuwa mwiba mchungu kwa kinara wa ODM Raila Odinga alisema haya wakati alikuwa akimkaribisha nyumbani kwake kijana ambaye alichangia pakubwa kampeni zake kwa kutunga wimbo ambao anahisi ndio uliwachochea wapiga kura kukubali sera zake.

Alisema kwamba kijana huyo alipata changamoto kuona nyumbani kwake ni safi na nadhifu licha ya mbunge huyo kutokuwa na mke.

Hata hivyo, Salasya alifichua kwamba ako na kijana wa kiume ambaye anamsaidia katika usafi wa nyumba yake.

“Mwanamuziki alishangaa kupata nyumba iliyopangwa vizuri isiyo na mke hehe ingawa nilimpa changamoto niko na house boy anafanya kazi ya ajabu,” Salasya alieleza.

Katika kipindi cha siku za hivi majuzi, Mbunge huyo amekuwa akikashifu ubia mpya baina ya rais William Ruto na kinara wa Azimio Raila Odinga.

Salasya hata hivyo amejipata akiburuzana mabega na baadhi ya wafuasi wa viongozi hao wawili, jambo ambalo hajalikalia kizembe.

Katika chapisho kwa njia ya video, Salasya aliwataka watu ambao bado wanaunga mkongo Raila Odinga kusitisha ufuasi katika kurasa zake za mitandao, akisisitiza haja ya kuwa na wafuasi wachache ambao wanafuata miongozo yake.

“Kama wewe ni mtu wa nyanza ama mufuasi wake na unaona sikubambi ebu unfollow me right now because you won’t have peace nitakupa depression. Nataka kubaki na wafuasi wachache ambao tunashiriki ideology ya kawaida ...lazima niwatoe ujinga wa huyu baba yenu ambaye amebadili akili zenu. Ametuchezea muda mrefu na lazima tumchezee sasa hivi,” Salasya alifoka.

Mbunge huyo hata alisema kwamba yuko tayari kupokea madhara yoyote yatakayotokana na msimamo wake wa kupinga ubia wa UDA na ODM.

Alisema kuwa haogopi kutolewa katika serikali hiyo jumuishi, akisema lengo ni kuhakikisha wananchi wanafahamu kile alichokitaja kama ukweli.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved