logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mike Sonko akanusha kuenda Vietnam kujadili kuachiliwa kwa Margret Nduta

Uvumi wa Sonko kuenda nchini Vietnam ulizuka TikTok baada ya yeye kuchapisha picha akiwa na raia kutoka China, jambo lililowafanya watu kudhani yuko Vietnam.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani18 March 2025 - 15:00

Muhtasari


  • Uvumi wa Sonko kuenda nchini Vietnam ulizuka TikTok baada ya yeye kuchapisha picha akiwa na raia kutoka bara la Asia, jambo lililowafanya watu kudhani yuko Vietnam.
  • Hata hivyo, alisema kwamba watu hao, japo wanafanana na raia wa Vietnam lakini ni wananchi wa Uchina ambao walimtembelea kwa mazungumzo ya kibiashara. 

Mike Sonko akiwa na raia wa China//X

GAVANA wa zamani wa Nairobi, Mike Sonko amekanusha uvumi kwamba amesafiri hadi nchini Vietnam kujadili uwezekano wa kuachiliwa kwa Mkenya Margaret Nduta dhidi ya hukumu ya kunyongwa.

Sonko alizungumza kupitia video ambayo alichapisha kwenye kurasa zake mitandaoni akikanusha uvumi huo na kikariri kwamba bado yuko Kenya.

Uvumi wa Sonko kuenda nchini Vietnam ulizuka TikTok baada ya yeye kuchapisha picha akiwa na raia kutoka bara la Asia, jambo lililowafanya watu kudhani yuko Vietnam.

Hata hivyo, alisema kwamba watu hao, japo wanafanana na raia wa Vietnam lakini ni wananchi wa Uchina ambao walimtembelea kwa mazungumzo ya ushirikiano wa kibiashara.

“Nimeona mtu kule TikTok akisema kwamba eti Sonko ametua nchini Vietnam kujadili kuachiliwa kwa Margaret Nduta, Mkenya aliyetarajiwa kunyongwa usiku wa jana. Atafanikiwa? Kila la heri,” chapisho hilo kwenye TikTok lilisomeka.

Sonko alicheka akisema kuwa huo ni mzaha uliotanuliwa nje ya mipaka, akisema kwamba yeye dawa ambazo anajihusisha nazo katika nyumba yake ni za kuzuia hatari za kiafya tu.

“Hii ni ile picha ya jana na hawa ni wawekezaji kutoka Uchina na sasa watu wanasema eti hapa ni Vietnam. Lakini hapa ni humu ndani ya nyumba yangu,” Sonko alieleza huku akifananisha mandhari ya picha hiyo na madhari sawia ya ndani ya nyumba yake walikopigia picha husika.

Mfanyibiashara huyo alimaliza kwa kutoa wito kwa serikali kufanya juhudi zote kuzuia hukumu ya Nduta kunyongwa na ikiwezekana kurejeshwa humu nchini.

Sonko alisema kwamba huenda msichana huyo alihadaiwa kubeba mzigo wa mtu ambaye baadae ulikuja kugundulika kuwa na chembechembe za dawa haramu nchini Vietnam, akitaka wahusika halisi kutafutwa.

“Hii kesi ya Margaret ni ndogo sana, inasemekana alibebea mtu kwa jina John dawa. DCI hebu tusaidie huyu msichana. Na njia pekee ya kumsaidia ni kutafuta mwenye alimsindikiza hadi uwanja wa ndege – pengine ni huyo John.”

“Tuangalie deta za namba ya simu ya mamake, alitoka Kenya lini, na kwa ile deta tutapata mwenye alimtuma Margaret na dawa, huyo ndio anafaa ashikwe apelekwe anyongwe, Margaret aachiliwe huru,” Sonko alieleza.

Nduta aliratibiwa kunyongwa usiku wa Jumatatu nchini Vietnam baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya.

Hata hivyo, serikali ya Kenya kupitia wizara ya masuala ya nje ilizungumza na Vietnam ambapo PS Korir Song’Oei aliwasiliana na mwenzako na kuahidiwa muda zaidi kushughulikia kesi hiyo ngumu.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved