logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bahati atangaza mpango wa kumnunulia Diana Marua Lamborghini baada ya Brabus

Mwishoni mwa Februari, Bahati alifanya kufuru ya karne kwa kumnunulia mkewe zawadi ya gari la pink la Brabus ambalo lilitajwa kuwa lenye thamani ya zaidi ya milioni 45 pesa za Kenya.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani14 April 2025 - 12:26

Muhtasari


  • Wawili hao walivalia mavazi ya waridi yaliyofanana, bila kujua kuwa mwanamuziki huyo alikuwa amenunua gari aina ya G-Wagon Brabus.
  • Bahati alifichua kuwa gari hilo lilikuwa na thamani ya KSh 45 milioni lilikuwa limeboreshwa kulingana na rangi ya waridi ya Diana.

Diana Marua, Bahati Kioko//Instagram

KEVIN Kioko maarufu kama Bahati ametangaza mpango wa kumnunulia mkewe, Diana Marua zawadi nyingine ya gari la kifahari.

Kupitia Instagram, Bahati alitoa maoni chini ya chapisho la Diana Marua ambaye alionyesha kuridhika na maisha anayopewa na mumewe kwa zawadi kochokocho.

Diana alionyesha gari aina ya Brabus ambalo Bahati alimpa wiki kadhaa zilizopita kama moja ya zawadi ya kusherehekea takribani muongo mmoja wa uhusiano wao.

“Diana Brabus, nitakuwa nadanganya kama nitasema maisha si mazuri,” Diana aliandika.

Akijibu, Bahati alisema kwamba gari hilo kwa vile limekuwa moja ya mada zilizozungumziwa sana katika mitandao ya kijamii, anapanga kumnunulia gari lingine la kifahari aina ya Lamborghini

“Hili gari limegonga vichwa vya habari sana, zawadi itakayofuata ni ya gari aina ya Lamborghini,” Bahati aliandika.

Mwishoni mwa Februari, Bahati alifanya kufuru ya karne kwa kumnunulia mkewe zawadi ya gari la pink la Brabus ambalo lilitajwa kuwa lenye thamani ya zaidi ya milioni 45 pesa za Kenya.

Gari hilo lilikuwa kelele cha jumla ya zawadi nane ambazo msanii huyo alimpa mkewe kama ishara ya kumshukuru na kumthamini kwa miaka 8 ya uhusiano wao ambapo wamebarikiwa na watoto 3.

Wawili hao walivalia mavazi ya waridi yaliyofanana, bila kujua kuwa mwanamuziki huyo alikuwa amenunua gari aina ya G-Wagon Brabus.

Bahati alifichua kuwa gari hilo lilikuwa na thamani ya KSh 45 milioni lilikuwa limeboreshwa kulingana na rangi ya waridi ya Diana.

Alianguka chini na kulia baada ya mumewe kufunua gari.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved