logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kwa nini hata nikiwa na mke na watoto bado mnaniuliza mbona mimi ni shoga – Mwanahabari wa 'Why Are You Gay?' ahoji

"Ninyi watu, mnanikuta na mke wangu na watoto halafu bado mnauliza, ‘Kwa nini wewe ni shoga?’ Kwa kweli?" Kaggwa alisema.

image
na Samuel Mainajournalist

Dakia-udaku28 March 2025 - 12:10

Muhtasari


  • Bw Kaggwa ameonyesha mshangao wake jinsi watu bado wanamuhusisha na swali hilo hata baada ya zaidi ya muongo mmoja kupita.
  • Bw Kaggwa, kwa mshangao na kejeli, alihoji kwa nini watu bado wanafikiria hivyo, akisisitiza ana mke aliyejaliwa watoto naye.

Simon Kaggwa Njala

Mtangazaji maarufu wa runinga kutoka Uganda, Simon Kaggwa Njala, anayejulikana sana kwa mahojiano yake ya kihistoria ya “Why are you gay?”, ameonyesha mshangao wake jinsi watu bado wanamuhusisha na swali hilo hata baada ya zaidi ya muongo mmoja kupita.

Kupitia chapisho kwenye mtandao wa X mnamo Alhamisi, Machi 27, mtangazaji huyo wa NBS TV alidokeza kuwa, licha ya kuwa na familia, bado anakutana na watu wanaomtania kwa kumwuliza, “Kwa nini wewe ni shoga?”.

Bw Kaggwa, kwa mshangao na kejeli, alihoji kwa nini watu bado wanafikiria hivyo, akisisitiza kuwa ana mke ambaye wamejaliwa watoto naye.

"Ninyi watu, mnanikuta na mke wangu na watoto halafu bado mnauliza, ‘Kwa nini wewe ni shoga?’ Kwa kweli?" Kaggwa aliandika.

Takriban miaka kumi na mitatu iliyopita, mtangazaji Simon Kaggwa Njala alimkaribisha mwanaharakati wa haki za binadamu wa Uganda Pepe Julian Onziema katika kipindi chake cha Morning Breeze kwenye runinga ya NBS ambapo walikuwa na mahojiano ya wazi kuhusu ushoga nchini Uganda.

Katika mahojiano hayo, Kaggwa alionekana kukerwa na sababu ya mwanaharakati huyo kuchagua kuwa shoga na alitaka sana kuelewa yeye ni nani hasa

"Why are you gay? (Kwa nini wewe ni shoga)?" Kaggwa aliuliza mara kwa mara huku mahojiano yakiendelea.

Onziema ambaye alizaliwa mwanamke hata hivyo hakutaka kuitwa shoga na kusisitiza kuwa yeye ni mwanamume anayevutiwa na wanamke.

"Mimi si mwanaharakati wa haki za binadamu anayetetea usawa kwa watu wenye mtazamo tofauti wa kimapenzi na ujinsia tofauti," alisema

Onziema pia alikiri kuwa na mpenzi mwanamke lakini akaweka wazi kuwa hakuwa akishiriki tendo la ndoa naye.

Alipuuzilia mbali madai kwamba alikuwa akipigia debe ushoga nchini Uganda na akakana kuwa alilipwa kufanya hivyo.

Mahojiano hayo magumu yalikuwa yakiendelea vizuri kabla ya Mchungaji Martin Ssempa ,ambaye ni mkosoaji mkubwa wa wapenzi wa jinsia moja, kuingia studio na kulaani mienendo ya Onziema. Punde baada ya kumuona Bw Ssemoa, mwanaharakati huyo  alisimama na kutoka nje lakini alishawishiwa na kurudi  baada ya muda mfupi.

Mahojiano hayo ya zaidi ya saa moja yamekuwa gumzo kwenye mitandao kwa miaka mingi iliyopita huku wanamitandao wakiyarejesha mara kwa mara.



Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved