logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Huna Hata Robo Ya Ujuzi Nilio Nao!” Sudi Amjibu Sifuna Kumwita ‘Class 2 Drop-Out’

“Mimi niko katika kiwango changu. Huna hata robo ya ujuzi wangu. Kwa hivyo usikuwe mpuuzi kuongea kama mtoto,” Sudi alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari20 February 2025 - 13:42

Muhtasari


  • Sudi alisema kwamba Sifuna amekuwa na hulka ya kushambulia kila mtu akidhani ni haki yake, lakini kwake amefika kwenye mwamba.
  • “Sio kuhusu shule, la maana ni kuwa na ujuzi. Sio kuhusu PhD, ni kuhusu hesabu. Mradi tu unaweza ona, unazungumza, unaweza ona na hata kunusa."

Edwin Sifuna na Oscar Sudi

VITA vya maneno kati ya mbunge wa Kapseret Oscar Sudi na Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna imeendelea kuchukua mikondo tofauti baada ya mbunge huyo kuruasha kombora katika kambi ya Sifuna.

Sifuna awali alikuwa amemkashifu Oscar Sudi akidai kwamba rais William Ruto anajishusha hadhi kuwa karibu na mbunge huyo.

Kwa mujibu wa Sifuna, rais Ruto anashusha hadhi yake kwa kutembea na Sudi ambaye alimtaja kama mtu mwenye ujuzi wa darasa la pili tu.

“Ruto alituambia kwamba ana PhD, mimi sijawahi ona mtu wa PhD anayetembea na mtu aliyeachia shule darasa la pili. Inawezekana aje wewe una PhD na unatembea na Sudi. Inawezekana aje hiyo kuwa ukweli,” Sifuna alisema katika mahojiano na runinga ya Citizen TV.

Tamko hili lilionekana kumuuma Sudi ambaye kupitia ukurasa wake wa X aliachia video akimzomea Sifuna.

Mbunge huyo wa Kapseret alisema kwamba Sifuna anaweza kuwa na elimu ya kiwango cha juu lakini katika ujuzi hafikii hata robo ya ujuzi wake yeye.

“Sifuna unaweza jilinganisha na mimi? Unajua IQ yangu na yako hazilingani hata kwa robo. Tafuta mtu mwingine ambaye unaweza jilinganisha naye au mwenye utalinganisha na Ruto,” Sudi alimwambia.

“Mimi niko katika kiwango changu na sio kwamba ninaringa au nini lakini unaweza ulizia kuhusu historia yangu. Huna hata robo ya ujuzi wangu. Kwa hivyo usikuwe mpuuzi kuongea kama mtoto,” Sudi aliongeza.

Sudi alisema kwamba Sifuna amekuwa na hulka ya kushambulia kila mtu akidhani ni haki yake, lakini kwake amefika kwenye mwamba.

“Sio kuhusu shule, la maana ni kuwa na ujuzi. Sio kuhusu PhD, ni kuhusu hesabu. Mradi tu unaweza ona, unazungumza, unaweza ona na hata kunusa… wewe sidhani uko na hizo zote. Wewe ni mtu tu bure, mpuuzi,” Sudi alimaliza.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved