logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Trump ananitii” Mwanawe Museveni ajigamba baada ya US kurejeshea Uganda msaada

Kainerugaba alidakia taarifa hiyo na kusema kwamba Marekani ilirejesha msaada wa matibabu ya UKIMWI Uganda kufuatia tweet yake siku chache nyuma akimtaka Trump kufanya hivyo.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari06 March 2025 - 08:34

Muhtasari


  • Mkuu huyo wa majeshi amekuwa mtu mwenye misimamo ya ajabu kupitia tweet zake katika mitandao wa X, huku akimshambulia mtu yeyote kwa wakati wowote anaoutaka yeye. 
  •  Wiki chache zilizopita, Muhoozi alikuwa akishambuliana na aliyekuwa mpenzi wa ujanani wa babake, Winnie Byanyima 

Muhoozi Kainerugaba, Donald Trump

MUHOOZI Kainerugaba, mwanawe rais Yoweri Museveni ambaye pia ni jenerali mkuu wa majeshi ya Uganda, UPDF amejitokeza kwen ye mitandao wa X kama kawaida yake na kudai kwamba rais wa Marekani Donald Trump anamsikliliza.

Hii ni baada ya balozi wa Uganda katika baraza la Umoja wa Mataifa, Adonia Ayebare kufichua kwamba serikali ya Marekani imerejesha misaada ya matibabu ya virusi vya HIV nchini Uganda.

Kainerugaba alidakia taarifa hiyo na kusema kwamba Marekani ilirejesha msaada wa matibabu ya UKIMWI Uganda kufuatia tweet yake siku chache nyuma akimtaka Trump kufanya hivyo.

“Ninataka kumuambia rais Donald Trump kurudisha msaada wa Marekani kwa wanaoathirika na virusi vya HIV nchini Uganda. Watu wetu watashukuru sana,” tweet hiyo ya Muhoozi siku 5 zilizopita ilisomeka.

Tweet ya Muhoozi

Kama sadfa vile, balozi huyo alifichua taarifa kwamba hatimaye Marekani imerejesha msaada huo kwa Uganda, Muhoozi alimshukuru balozi huyo kwa kuhakikisha hilo lakini pia akamshukuru Trump kwa kusikiliza ombi lake la awali.

“Nimefahamu kutoka kwa Balozi @adoniaayebare kwamba serikali ya Marekani imerejesha usaidizi wote wa VVU/UKIMWI kwa Kituo cha Utafiti wa Kitabibu cha Pamoja (JCRC) baada ya tweet yangu siku chache zilizopita. Namshukuru Rais @realDonaldTrump na serikali yake kwa kuwa upande sahihi wa historia na kusaidia watu wetu! Pia nashukuru @USAmbUganda William Papa kwa kazi yake nzuri katika kurejesha usaidizi huu. Mwisho namshukuru Balozi @adoniaayebare kwa kuratibu juhudi hizi,” Muhoozi Kainerugaba alisema.

Mkuu huyo wa majeshi amekuwa mtu mwenye misimamo ya ajabu kupitia tweet zake katika mitandao wa X, huku akimshambulia mtu yeyote kwa wakati wowote anaoutaka yeye.

Wiki chache zilizopita, Muhoozi alikuwa akishambuliana na aliyekuwa mpenzi wa ujanani wa babake, Winnie Byanyima – ambaye sasa ni mke wa mwanasiasa wa upinzani Kizza Besigye.

Wiki hii, Muhoozi amekuwa akishambulia moja ya gazeti maarufu la humu nchini baada ya jarida hilo kuchapisha stori yake kwenye ukurasa wa mbele katika moja ya toleo la wikendi iliyopita.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved