logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gavana Arati aahidi Sh100k kwa yeyote atakayekamata na kuchoma mwizi mpakani

“Mkichoma mniambie gavana tulichoma mwizi hapa Trans Mara, ama hapa Kisii, Nitapeana shilingi elfu 100 kwa kuchoma mwizi. Hata hao wezi wakiwa 10,” Arati alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari11 March 2025 - 08:52

Muhtasari


  • “Mkichoma mniambie gavana tulichoma mwizi hapa Trans Mara, ama hapa Kisii, na huyo yuko hospitalini anapona. Nitapeana shilingi elfu 100 kwa kuchoma mwizi."
  • “Hata hao wezi wakiwa 10, niko tayari kutoa shilingi milioni moja. Unajua wakati mwingine tunacheza na moto sana." 

Simba Arati, gavana wa Kisii

GAVANA wa Kisii, Simba Arati ametoa ahadi ya shilingi laki moja kwa yeyote atakayemkatama na kumchoma mwizi wa mifugo katika mpaka wa Kisii na Narok.

Akizungumza Jumatatu katika eneo la mpakani mwa Bomachoge Borabu na Trans Mara wakati wa mkutano wa kutafuta suluhu ya amani uliowakutanisha wananchi na viongozi kutoka jamii za Abagusii na Maasai, Arati alisema kwamba ni sharti suluhu dhidi ya wizi wa mifugo lipatikane na liwe la kudumu.

Gavana huyo alitoa ahadi kwa wananchi kumkamata mwizi wa mifugo na kumteketeza katika eneo hilo la mpaka na pindi taarifa hizo zitakapomfikia, atatoa kima cha shilingi 100k.

“Mkichoma mniambie gavana tulichoma mwizi hapa Trans Mara, ama hapa Kisii, na huyo yuko hospitalini anapona. Nitapeana shilingi elfu 100 kwa kuchoma mwizi. Hiyo biashara ndio tumalize,” Arati alisema.

“Hata hao wezi wakiwa 10, niko tayari kutoa shilingi milioni moja. Unajua wakati mwingine tunacheza na moto sana. Mtoto anaangusha moto hapa na nyumba yote inashika moto. Hatutaki biashara kama hiyo. Kuanzia sasa mimi niko tayari,” gavana huyo aliongeza.

Kiongozi huyo ambaye ni naibu wa chama cha ODM alisema kwamba hata gavana mwenzake wa Narok, Patrick Ole Ntuntu ameafiki na hilo, akisema kwamba wakati mwizi atachomwa atachangia hela kuwatunuku vijana.

‘Hata huyo ni mtu ako na pesa, gavana usijali nikikufikia nikwambie kwamba nimefika milioni moja au mbili tumechoma wezi 20, wewe utaniongeza milioni nyingine tukawape watu kwa kazi nzuri. Kwa sababu hakuna haja ya kuzungushana namna hii, watoto wanafaa kuwa shuleni, lakini eti kwa sababu ya vita watoto hawawezi enda kusoma. Kina mama ambao wamepanda mboga pande hii hawawezi peleka mboga sokoni, hii upuzi lazima iishe,” Arati alitema moto.

Vita baina ya jamii hizo mbili vimekuwa kwa takribani wiki mbili sasa chanzo kikisemekana kuwa ni kuibwa kwa ng’ombe wawili.

Makumi ya vijana wamejeruhiwa huku takribani 3 wakiripotiwa kufa kutokana na majeraha ya mishale na panga.

Jumatatu, waziri wa masuala ya ndani Kipchumba Murkomen alitoa onyo kali kwa watu wanaotembea na silaha katika eneo hilo la mpakani akisema kwamba vyombo vya dola vitaanza sakasaka za kuwakamata wote watakaopatikana wakizurura na silaha.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved