logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila aliua KANU na UDA hakuna mahali inaenda, 2026 mwisho atatoka na kila mtu – Okanga

Okanga anahisi kwamba Odinga kukubali ODM kufanya kazi na chama tawala cha UDA kumewaacha wafuasi wake wengi katika hali ya kuchanganyikiwa.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari06 April 2025 - 13:12

Muhtasari


  • Okanga anahisi kwamba Odinga kukubali ODM kufanya kazi na chama tawala cha UDA kumewaacha wafuasi wake wengi katika hali ya kuchanganyikiwa.
  • Okanga alitabiri kwamba Odinga atafanya vivyo hivyo kwani ataondoka na kila mwishoni mwa 2026 na kuacha UDA kikiwa bila ushawishi wowote wa kisiasa kuelekea uchaguzi wa 2027.

Nuru Okanga, Raila Odinga//FACEBOOK

MWANASIASA anayechipukia, Nuru Okanga amedai kwamba yeye kama mmoja wa wakereketwa wa sera za kinara wa ODM, Raila Odinga amebaki katika njia panda baada ya kiongozi huyo kuingia katika ubia na rais Ruto.


Okanga anahisi kwamba Odinga kukubali ODM kufanya kazi na chama tawala cha UDA kumewaacha wafuasi wake wengi katika hali ya kuchanganyikiwa.


“Mimi ni mtu wa Raila Odinga na nakubaliana na hilo, lakini Baba kwa kweli anatuchanganya. Juzi akiwa katika mazishi huko Mlima Kenya alisema kuwa hayuko kwa serikali. Sasa lini ndio lipi? ako wapi?” Okanga alisema.


Licha ya kukiri kuchanganyikiwa na hatua hiyo, Okanga alisema mkubwa haulizwi swali na kudai kwamba kwa wale wanaojua siasa za kinara huyo, wanajua kwamba kuungana kwake na serikali ni moja ya mbinu za kufifisha ushawishi wa chama tawala, UDA.


Alitolea mfano jinsi Odinga aliunmgana na hayati Moi mwaka wa 1999 na miaka miwili baadae kuelekea uchaguzi wa 2002, alikififisha chana cha KANU kwa kuondoka na kila mtu na kutangaza ‘Kibaki tosha’.


Okanga alitabiri kwamba Odinga atafanya vivyo hivyo kwani ataondoka na kila mwishoni mwa 2026 na kuacha UDA kikiwa bila ushawishi wowote wa kisiasa kuelekea uchaguzi wa 2027.


“Tumemuachia hiyo nafasi, wacha acheze huo mpira, na tunajua Baba venye anacheza siasa yake sababu yeye aliua KANU. Hiki chama cha UDA hakuna mahali kinaenda. Baba atatoka na timu yote 2026 ikikaribia mwisho tukikaribia uchaguzi,” Okanga alidai.


Mwezi jana, Odinga alitia saini ya ubia mpya kati ya chama cha ODM na UDA katika kile alichokisema kwamba ni hatua ya kutuliza joto la siasa humu nchini ili kutoa nafasi kwa rais kufanya kazi.


Ni ubia ambao Ruto amekuwa akiupigia debe katika ziara zake Maeneo mbalimbali akisema kwamba ni hatua nzuri ambayo itaona Maeneo mengi yakipokea maendeleo kwani hakutakuwa na siasa.


Ambacho kila mtu anasubiria ni je, ubia kati ya Odinga na Ruto utadumu kwa muda upi?


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved