
Mahakama Kuu ya Kimataifa ilisema siku ya Ijumaa itasikiliza kesi iliyoletwa na Sudan kutaka hatua za dharura zichukuliwe dhidi ya Umoja wa Falme za Kiarabu na kuishutumu nchi hiyo ya Ghuba kwa kukiuka majukumu chini ya Mkataba wa Mauaji ya Kimbari kwa kuvipa silaha vikosi vya kijeshi.
Sudan imeishutumu UAE kwa kuwapa silaha wanajeshi wa Kikosi cha wanamgambo wa RSF ambacho kimekuwa kikipigana na jeshi la Sudan katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa muda wa miaka miwili, madai ambayo UAE inakanusha.
''Hatua ya Jeshi la Sudan katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) ni ''mchezo wa kisiasa, na jitihada la kumburuza katika mzozo rafiki wa Afrika kwenye mzozo ambao wenyewe wameuanzisha na kuuchochea," afisa wa UAE alisema.
"Pamoja na hayo, UAE inasalia imara katika ahadi yake ya kibinadamu kwa watu wa Sudan, inayolenga kupunguza maafa ya kibinadamu yaliyosababishwa na pande zote mbili zinazopigana."
Malalamiko ya Sudan kwa ICJ yenye makao yake The Hague, yanahusiana na mashambulizi makali ya kikabila yaliyofanywa na RSF na wanamgambo washirika wa Kiarabu dhidi ya kabila lisilo la Kiarabu la Masalit mwaka 2023 huko Darfur Magharibi.
Sudan imeomba mahakama ichukue hatua za dharura kuamuru Emirates kuzuia vitendo vya mauaji ya halaiki huko Darfur.
Mahakama ilisema itasikiliza ombi la Sudan tarehe 10 Aprili.