logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa mwanhabari Moses Dola achiliwa baada ya miaka 10 jela kwa mauaji ya mkewe

Dola, alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 10 kwa mauaji ya mkewe, Sarah Wambui Kabiru, 2011, mwanahabari mwenzake.

image
na Davis Ojiambo

Mahakama06 March 2025 - 14:28

Muhtasari


  • Alipatikana na hatia ya kuua bila kukusudia mwaka wa 2018 baada ya mahakama kupata kwamba Wambui alifariki kufuatia ugomvi wa nyumbani.
  • Dola, alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 10 kwa mauaji ya mkewe, Sarah Wambui Kabiru, 2011, mwanahabari mwenzake.
  • Akiwa gerezani Dola ajiunga na kozi ya uanasheria, na tayari amejisajili kwa cha Sheria nchini (KSL).

Aliyekuwa mwanahabari Moses Dola (Kushoto) akiwa kizimbani, marehemu mkewe Wambui Kabiru (Kulia)..

Mwanahabari Moses Dola Otieno ameachiliwa huru baada ya Jaji wa Mahakama ya Juu Alexander Muteti kukubali ombi lake la kutathmnii upya hukumu yake.

Mahakama hiyo pia iliagiza idara ya magereza kumwachilia mara moja isipokuwa azuiliwe kwa kosa lingine.

Uamuzi huo ulitolewa kwa njia video, ambapo Dola alitoa shukrani kwa hakimu na kushiriki matumaini yake ya kufika mbele yake tena baada ya kumaliza mafunzo yake ya uanasheria.

Dola, alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 10 kwa mauaji ya mkewe, Sarah Wambui Kabiru, 2011, mwanahabari mwenzake.

Alipatikana na hatia ya kuua bila kukusudia mwaka wa 2018 baada ya mahakama kupata kwamba Wambui alifariki kufuatia ugomvi wa nyumbani kwao jijini Nairobi. Dola baadaye alijisalimisha kwa mamlaka baada ya kujificha.

Akiwa gerezani Dola ajiunga na kozi ya uanasheria, na tayari amejisajili kwa cha Sheria nchini (KSL).

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved