
MHALIFU wa kingono ambaye alichukua kwa siri karibu picha 800 za wanaume wanaotumia vyoo amefungwa jela.
Chleo Sunter, 37, alinaswa akiwa na picha 790 na video 15 za
wanaume wakiwa ndani ya vyoo na wakiwa wamesimama kwenye sehemu za kujisaidia
haja ndogo.
Alichukua picha hizo akiwa amevaa nguo za wanaume kwenye duka
kuu la Aldi, kituo cha ununuzi huko Middlesbrough, na katika Kituo cha Treni
cha Darlington nchini Uingereza kati ya Januari na Novemba 2023.
Kwa mujibu wa Metrok UK, Sunter ambaye awali alijulikana kama
John Leslie Graham, alikiri kwa makosa mawili ya voyeurism (mazoea ya kupata
raha ya kimapenzi kutokana na kuwatazama wengine wanapokuwa uchi au wanashiriki
tendo la ndoa) katika katika mahakama ya jiji.
Pia alikiri ukiukaji sita wa amri ya kuzuia madhara ya
kufanya mapenzi baada ya kupatikana kuwa na picha uchi mwaka wa 2014 wakati
Sunter alipoitwa John Leslie Graham.
Sunter alinaswa na nyenzo hiyo wakati meneja wake
aliyemdhulumu kimapenzi alipofika nyumbani kwake huko Thornaby, ili kuangalia
kama alikuwa akifuata amri ya mahakama.
Picha na video za wahasiriwa wanaotumia vifaa vya umma karibu
na kituo cha ununuzi cha Captain Cook Square cha Middlesbrough, Middlesbrough
Aldi; na katika kituo cha Darlington, zilihifadhiwa kwenye simu yake.
Wachunguzi wa polisi waligundua kuwa alikuwa amefuta
mazungumzo 695, picha 712 na video nne kutoka kwa programu ya uchumba ya
mashoga, mahakama ilisikia.
Sunter pia amekuwa akitumia simu yake katika hali fiche ili
historia yake ya matumizi ya mtandao isionekane.
Wakili wa Sunter alimwomba hakimu azingatie amri ya mahakama
badala ya jela - akisema kwamba kufungwa kungemaanisha kwamba atapoteza makao
yake na kukabiliwa na ukosefu wa makazi atakapoachiliwa.
Jaji alisema anafahamu matatizo ya afya ya akili ya Sunter na
‘hali maalum, lakini yana madhara kidogo au hayana madhara yoyote’.
Jaji huyo alimfunga jela Sunter, kwa miezi 26, akimwambia
kwamba anakubali kwamba alikuwa 'mwenye mazingira magumu kihisia.