logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hatima ya Sifuna kama katibu mkuu wa ODM iko katika njia panda, mzozo ukizidi kutokota

Bwana Aladwa katika matamshi yake alidai kuwa bwana Sifuna ni kibaraka wa aliyekuwa naibu wa rais bwana Rigathi Gachagua na kusema kuwa njama yake ni kuwania kiti cha Ugavana Nairobi

image
na Evans Omoto

Yanayojiri25 February 2025 - 11:31

Muhtasari


  • Mbunge wa Makadara mheshimiwa George Aladwa ambaye pia ndiye mwenyekiti wa ODM tawi la Nairobi alinukuliwa akimkashifu bwana Sifuna kwa kuwa na hulka ya kupinga sera za chama na azima ilihali yeye ni katibu mkuu chamani.

Edwin Sifuna

 Hatima ya Katibu mkuu wa ODM Edwin Sifuna iko katika mizani ya kuondolewa au kusalia chamani.

Hii ilitokea baada ya wanachama wa ODM kumsuta wakisema kuwa kwa muda mrefu ameonekana kupinga sera na maendeleo ya chama.

Mbunge wa Makadara mheshimiwa George Aladwa ambaye pia ndiye mwenyekiti wa ODM tawi la Nairobi alinukuliwa akimkashifu bwana Sifuna kwa kuwa na hulka ya kupinga sera za chama na azima ilihali yeye ni katibu mkuu chamani.

Bwana Aladwa katika matamshi yake alidai kuwa  bwana Sifuna ni kibaraka wa aliyekuwa naibu wa rais bwana Rigathi Gachagua na kusema kuwa njama yake ni kuwania kiti cha Ugavana Nairobi akishirikiana na mheshimiwa Gachagua.

’Tunataka kumwambia bwana Sifuna aache kujipiga kifua awaheshimu viongozi wengine sisi kama viongozi wa ODM tuna heshima, hatutukani viongozi wengine katika Runinga hata kama ulisoma usitukane wale ambao hawakusoma baadala yake anzisha kampuni yako ya sheria na uwachane na chama’’ mheshimiwa Aladwa lieleza.

Chama cha ODM kinaonekana kupasuka Katikati kufuatia kwa bwana Odinga kupoteza nafasi katika nafasi ya uwenyekiti AUC hivyo kufanya wanachama Fulani kuunga mkono serikali ya Kenya Kwanza na wengine wakionekana kukosoa ukuruba kati ya bwana Odinga na Rais Ruto.

Kwa upande mwingine Gavana wa Homabay Gladys Wanga kwa upande wake alielezea hisia zake akisema kuwa wakati ambapo walikuwa wakihuzunukia kupoteza ushindi wa AUC wakiwa katika mji wa Addis Ababa nchini Uhabeshi(Ethiopia) alisema kuwa kulikuwa na Wakenya Fulani kutoka sehemu za nchi walikuwa wakifurahia kufeli kwa Bwana Odinga.

’Wakati ambapo tunalia kule vichochoroni kwa kupoteza nafasi ya AUC watu wengine wanafurahia, wanacheka na kuinua miguu juu tukasema ni sawa tu tumejua marafiki zetu ni nani na maadui zetu ni nani’’. Bi Wanga alisema.

Haya yanapojiri wito wa wanachama wa ODM wanazidi kurai chama kijitose mzimamzima kwa makubaliano na chama cha Kenya kwanza kwa kushirikiana.

Siku ya Jumatatu Februari 24,2025 kiongozi wa ODM bwana Odinga alikutana na Kiongozi wa Taifa Rais William Ruto Katika ikulu ndogo ya Mombasa ambapo walilakiana na kukaribishwa nyumbani  bwana Odinga baada ya kupoteza wadhifa wa mwenyekiti wa AUC.

Hata hivyo bwana Odinga alikanusha madai kuwa serikali ilitumia mabilioni ya hela katika kampeni yake,aliahidi kutoa mwelekeo wao kama chama siku za hivi karibuni.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved