logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Matamshi ya Gachagua yamlikwa kwa kumtetea Jaji Mkuu Martha Koome

Matamshi ya aliyekuwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua ya kumtetea jaji mkuu Matha Koome yaliibua tetesi nyingi miongoni mwa viongozi.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri25 February 2025 - 12:43

Muhtasari


  • Siku ya Jumapili ya tarehe 23,2025 Rigathi Gachagua akiwa Kaunti ya Meru katika hafla ya umma aliweza kutoa madai kuwa anafahamu njama iliokuwa ikipangwa na serikali ili kumuondoa Jaji mkuu Maatha Koome afisini.

CJ Martha Koome

Matamshi ya aliyekuwa Naibu wa Rais Bwana Rigathi Gachagua ya  kumtetea jaji mkuu Martha Koome yaliibua tetesi nyingi miongoni mwa viongozi.

Siku ya Jumapili ya tarehe 23,2025 Rigathi Gachagua akiwa Kaunti ya Meru katika hafla ya umma aliweza kutoa madai kuwa anafahamu njama iliokuwa ikipangwa na serikali ili kumuondoa Jaji mkuu Maatha Koome afisini.

Kwa kujibu kauli hiyo ya Gachagua naibu wa Rais Kithure Kindiki katika chapisho kwenye mtandao wake wa X aliweza kusema kuwa suala la kupata nafasi kama jaji mkuu au kuondolewa si jambo la siasa bali ni jambo la kikatiba na ambalo hufuta taratibu za Katiba na Sheria.

Seneta wa Makueni Dan Maanzo katika usemi wake alipohojiwa na kituo kimoja cha runinga nchini aliweka mambo paruwanja kwa kusema kuwa hilo jambo la kutaka kumuondoa jaji mkuu Martha Koome si jambo la siri ila ni jambo ambalo linajulikana.

Alifafanua  akisema kuwa si mara moja au mbili aliwahi kuraiwa na viongozi wa kutoka mrengo wa Kenya Kwanza wakihitaji huduma zake ili kuasisi mchakato huo wa kuwang’atua majaji afisini.

Alielezea kwa kusema kuwa hilo ni jambo ambalo huchukua mkondo wa siasa kwa hivyo ikiwa ulichaguliwa kutokana na nguvu za kisiasa bila shaka kuwa tayari kundolewa  kisiasa ,alieleza kuwa mara nyingi mambo hayo huchukua mkondo wa siasa.

Kwa upande wake Seneta Richard Onyonka naye alisema kuwa matamshi ya bwana Gachagua ya kusema kuwa iwapo rais Ruto ataitikia Martha Koome kuondolewa  asikanyage Meru ni tamko la kuleta chuki na uhasama akisema kuwa kwa Bahati mbaya jambo baya limtendekee rais  akiwa huko itakuwa vipi au itasemekana vipi.

Kwa upande mwingine mbunge wa Kimilili Mheshimiwa Didimus Barasa katika ukurasa wake wa X aliweza kutilia doa hali ya Jaji Koome kusalia kimya huku Rigathi  Gachagua akiwa ndiye anayemtetea ni nani kwa nini atetewe ilihali jaja anafahamu kazi yake ambayo imo katika  misingi ya Katiba?

Kwa upande mwingine mheshimiwa Gakuya alinukuliwa akimtetea Gachagua kwa kusema kuwa wabunge kutoka jamii ya Mulembe bungeni kuna mbunge aliyetetea spika Wetang’ula kutoguswa kwa vyovyote vile ilihali Gachagua akitetea wa kwao wanamsuta  eti ni mkabila.

Hata hivyo jambo la kuondoa jaji mkuu au kusalia  afisini ni jambo la kisheria ambalo linaipa tume ya JSC kutekeleza wajibu huo pasi na kuingiliwa na wanasiasa au watu wenye nia ya kusambaratisha haki na uhuru wa mahakama.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved