logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Huwezi Ku’hit Kwa Kuimba Kama WaTZ” – Cassypool Asuta Kolabo Za Bahati Na Pozee

Cassypool alisema kwamba wawili hao wanajaribu kuimba Watanzania katika uimbaji, kitu ambacho kinakwamisha ngoma zao kutoka katika ubora unaostahili.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani05 February 2025 - 12:14

Muhtasari


  • Kwa mujibu wa Cassypool, ngoma za wawili hao haziwezi kuwa pendwa kwa mashabiki wengi zaidi ya wiki moja kwa sababu zinaiga ladha za kigeni.
  • Cassypool aliipigia chapuo Gengetone na Arbantone kwamba ndizo zitateka anga za mawimbi ya muziki wa Kenya kwani nfizo ngoma zenye ladha halisi ya humu nchini.

caption

CASSYPOOL amejiunga na Weezdom kukejeli kolabo mbili zilizoachiliwa na wasanii Bahati na Willy Paul baada ya kujenga upya urafiki wao.

Akizungumza na mtengenezaji wa maudhui Trudy Kitui, Cassypool alisema kwamba hakuna msanii wa Kenya anaweza faulu kwa kuimba jinsi wawili hao wanaimba.

Kwa mujibu wa Cassypool, ngoma za ‘Keki’ na ‘Paah’ zilizofanywa kikoa na Bahati na Willy Paul na kuachiliwa Ijumaa iliyopita si kingine zaidi ya takataka.

Cassypool alisema kwamba wawili hao wanajaribu kuimba Watanzania katika uimbaji, kitu ambacho kinakwamisha ngoma zao kutoka katika ubora unaostahili.

“Mimi nilisema huwezi kuimba kama Mbongo na uhit. Haiwezekani. Unaimba kama Diamond na unataka ku’hit eti tukuje tukusifiwe eti umetoa ngoma kubwa. Hiyo ni kuharibu wakati; ni takataka. Ni nini hiyo waliimba?” Cassypool alisema.

Kwa mujibu wa Cassypool, ngoma za wawili hao haziwezi kuwa pendwa kwa mashabiki wengi zaidi ya wiki moja kwa sababu zinaiga ladha za kigeni.

Cassypool aliipigia chapuo Gengetone na Arbantone kwamba ndizo zitateka anga za mawimbi ya muziki wa Kenya kwani nfizo ngoma zenye ladha halisi ya humu nchini.

“Huwezi kuimba ngoma ambazo zina’hit kwa wiki moja tu. Gengetone ndio inateka anga. Lakini ukituwekea vijana wawili mmoja amebeba kifua mawe yamelala upande mmoja na kifua imelala huku kwingine halafu mwingine anaimba kwa sauti ya soprano kama mwanamke na kutuambia hao ndio wasanii ni kazi bure,” Cassypool alisema.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved