logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond Atafunga Harusi na Zuchu, Sherehe Yao Kutachinjwa Ngamia 21 – Rafikiye

Chawa huyo alisema kuwa harusi ya Diamond na Zuchu itafanya ile ya Hamisa Mobetto na Aziz Ki kuonekana kama mzaha kwani sherehe yao itafanyika kwa siku 17 mfululizo.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani18 February 2025 - 12:19

Muhtasari


  • Akijibu kuhusu ni kwa nini anahisi Diamond amechukua muda mrefu kumuoa rasmi Zuchu, Baba Levo alisema;
  • “Watu hawaoani kwa kukurupuka, watu hawaoani kwa kuigiza. Watu wanaoana kwa sababu ya mapenzi na mpango uliopangwa.”

Diamond na Zuchu wadokezwa kupanga harusi yao, sherehe kufanyika siku 17 ngamia 21c kuchinjwa

RAFIKI na mwandani wa msanii Diamond Platnumz, Baba Levo amefichua kwamba msanii huyo ana mpango kabambe wa kulisimamisha jiji kwa harusi yake na Zuchu.

Akizungumza na waandishi wa habari siku moja baada ya harusi ya kipekee na mwanamitindo Hamisa Mobetto na mkwanasoka wa Yanga SC kutoka Burkina Faso, Stephane Aziz Ki, Levo alisema kuwa Diamond ameanzisha mipango kufanikisha jambo lake.

Chawa huyo alisema kuwa harusi ya Diamond na Zuchu itafanya ile ya Hamisa Mobetto na Aziz Ki kuonekana kama mzaha kwani sherehe yao itafanyika kwa siku 17 mfululizo, watu wakifurahia kitoweo cha nyama ya ngamia 21 ambao watatiwa visu.

“Diamond Platnumz atamuoa Zuchu na mpango uliopo ambao nimeamua kuwapa kwa sababu ilitakiwa iwe siri ambayo nilikuwa nimeificha ni kwamba watachinjwa ngamia 21 kwenye harusi hiyo.”

“Ngamia wataangushwa wa kutosha, watu wale na sherehe zitakuwa kwa siku 17 mfululizo, kila mkoa watapata nafasi ya kusherehekea harusi ya Zuchu na Diamond, hivyo tulieni msiwe na wasiwasi,’ Baba Levo alisema.

Akijibu kuhusu ni kwa nini anahisi Diamond amechukua muda mrefu kumuoa rasmi Zuchu, Baba Levo alisema;

“Watu hawaoani kwa kukurupuka, watu hawaoani kwa kuigiza. Watu wanaoana kwa sababu ya mapenzi na mpango uliopangwa.”

Mtunza siri huyo wa Diamond Platnumz alionekana kuipuzilia mbali harusi ya aliyekuwa ex wa bosi wake, Hamisa Mobetto akisema kuwa hiyo yao hata haifai kufananishwa hata kidogo na harusi ya msanii wa Nigeria, Davido.

Wikendi iliyopita, Hamisa na Aziz Ki walifunga harusi baada ya kukamilika kwa taratibu zac ulipaji mahari, shughuli iliyofanyika katika jiji la kibiashara la Dar es Salaam.

Licha ya sekeseke kuibuka kwamba mwanasoka huyo alilipa mahari ya ng’ombe 30, mamake Mobetto alikanusha taarifa hizo na kunyoosha maelezo kwamba Aziz Ki alilipa mahari ya jumloa ya ng’ombe 150 pamoja na kiasi cha fedha ambacho alisita kukitaja.

Diamond na Zuchu wamekuwa wakisemekana kuwa katika huba zito tangu mapema 2022 ambapo mara ya kwanza walitania kufunga harusi ilikuwa kuelekea siku ya wapendanao ya mwaka huo.

 

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved