logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watanzania Wanapenda Wasanii Wote Wa Kenya Isipokuwa Tu Willy Paul – Bien

“Nchini Tanzania sio tu Bien pekee, kila mtu anapendwa kule isipokuwa Willy Paul,” Bien alisema huku akitania

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani03 March 2025 - 10:49

Muhtasari


  • “Nchini Tanzania sio tu Bien pekee, kila mtu anapendwa kule isipokuwa Willy Paul,” Bien alisema huku akitania
  • Willy Paul alijizolea idadi kubwa ya maadui mwishoni mwa mwaka jana alipozua mtafaruku baina yake na baadhi ya wasanii kutoka Tanzania katika tamasha la Raha Fest. 

Willy Paul na Bien

MSANII bora wa Afrika Mashariki mwaka huu kwa mujibu wa tuzo za Trace, Bien Baraza amewapongeza raia wa taifa jirani la Tanzania kwa kuwa watu wenye mapenzi ya hali ya juu kwa wasanii kutoka Kenya.

Akizungumza wikendi iliyopita katika mwendelezo wa mbwembwe za kusherehekea ushindi wake dhidi ya wababe kama kina Diamond na kuibuka msanii bora Afrika Mashariki, Bien alisema kwamba kila mara anapokuwa nchini Tanzania, yeye hujihisi kama vile yuko nyumbani.

Msanii huyo anayezidi kutamba kwa kolabo yake na Marioo kutoka Tanzania ya Nairobi alisema kwamba watu wa Tanzania wanawapenda wasanii wa Kenya lakini akatilia mashaka kama mapenzi hayo yanafika hadi kwa Willy Paul.

“Watanzania wanatusapoti sana na ukweli ni kwamba wasanii wetu wanapata kuheshimiana kwingineko pia kwa sababu mara nyingi unapata sisi tunawapenda wengine na hayo mapenzi yanarudishwa kwetu.”

“Nchini Tanzania sio tu Bien pekee, kila mtu anapendwa kule isipokuwa Willy Paul,” Bien alisema huku akitania kwamba kama Watanzania wangependa aishi vizuri nchini mwao basi wampe mke na nyumba nzuri.

Willy Paul alijizolea idadi kubwa ya maadui mwishoni mwa mwaka jana alipozua mtafaruku baina yake na baadhi ya wasanii kutoka Tanzania katika tamasha la Raha Fest.

Pozee aliripotiwa kukejeli kolabo yake na Rayvanny – Mmmh kwa kuiita ‘takataka’ pindi ilipochezwa akiwa jukwaani kutumbuiza, kisha akaamrisha itolewe mara moja.

Awali, alikuwa amedaiwa kuzua mtafaruku baina yake na Diamond Platnumz ambaye alitarajiwa kutumbuiza lakini hakuweza kutumbuiza katika kile alichokitaja baadae kama ukosefu wa usalama wa kutosha.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved