logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Good English for who?” Harmonize awasuta wanaodai anaboronga Kiingereza vibaya mno!

“Ukiona hujaelewa ina maana wazo hilo halikukusudiwa kwako. Mimi ndiye msanii pekee kutoka Afrika Mashariki anayeimba kwa Kiingereza, chukua hilo!” Harmonize alidai.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani18 April 2025 - 14:15

Muhtasari


  • Harmonize aliweka wazi kwamba hababaishwi na wale wanaocheka umahiri wake katika lugha ya Kiingereza, akisema kwamba ataendelea kukizungumza kwa jinsi anataka mwenyewe.
  • Aidha, alisema kwamba wale wanaosema Kiingereza chake ni kibovu, ni kibovu tu kwao lakini kwa yeye mwenyewe na wengine ambao wanamuelewa, Kiingereza chake mbona kimenyooka tu!

Harmonize awasuta wanaodai Kiingereza chake ni kibaya//INSTAGRAM

KWA mara nyingine, Harmonize amevunja kimya kwa kejeli nyingi dhidi ya jitihada zake za si tu kuzungumza bali pia kuimba kwa lugha ya mkopo – Kiingereza.

Katika chapisho kwenye ukurasa wake wa Instagram, Harmonize alifichua kwamba amekuwa akiona dharau hizo dhidi ya Kiingereza chake lakini amekuwa akipuuza, na sasa ni muda wa kuwajibu wanaokejeli matamshi yake kwa Kiingereza.

Harmonize aliweka wazi kwamba hababaishwi na wale wanaocheka umahiri wake katika lugha ya Kiingereza, akisema kwamba ataendelea kukizungumza kwa jinsi anataka mwenyewe.

Aidha, alisema kwamba wale wanaosema Kiingereza chake ni kibovu, ni kibovu tu kwao lakini kwa yeye mwenyewe na wengine ambao wanamuelewa, Kiingereza chake mbona kimenyooka tu!

“Sasa acheni niwafanye nyinyi wote muelewe na tafadhali nifafanulieni, kwa nini nizungumze Kiingereza sahihi? Kwa ajili ya nani? Kwa nia gani chale wangu?”

“Angalia, Kiingereza changu siku zote kiwakuwa kibaya kwako na hata sitishiki na hilo hata kidogo,” alisema.

Msanii huyo alisema kwamba wale wanaodai hawaelewi anachoimba katika nyimbo zake za Kiingereza wanastahili kujiondoa kwenye mlolongo na kuwapisha wenye ujumbe umekusudiwa, kwani kama humuelewi basi ujumbe si wa kwako.

Pia alimaliza kwa kujitapa kwamba yeye ndiye msanii pekee kutoka Afrika Mashariki nzima anayeimba kwa lugha ya Kiingereza, kauli ambayo inawatupa baharini wasanii wenzake wanaofanya vizuri kwa miziki ya Kiingereza kutoka Kenya na Uganda.

“Ukiona hujaelewa ina maana wazo hilo halikukusudiwa kwako. Mimi ndiye msanii pekee kutoka Afrika Mashariki anayeimba kwa Kiingereza, chukua hilo!” Harmonize alidai.

Kauli ya Harmonizr kwa wanaokejeli Kiingereza chake//INSTAGRAM

Awali, Harmonize alijitetea kwamba yeye ndiye msanii pekee kutokea Tanzania ambaye wimbo wake umetambulika kimataifa na ambao uliimbwa kwa 90% Kiingereza.

Bila shaka, hapa alikuwa anarejelea wimbo wake wa ‘Single Again’ ambao kusema kweli ulikuwa bonge la hit ambayo iliwavutia watu kadhaa kutoka ndani ya nje ya Afrika.

Akisherehekea mafanikio hayo, Harmonize alifichua kwamba yeye ana elimu ya darasa la 7 tu na kwamba Kiingereza chote anachokiimba na kukizungumza hajafunzwa na mtu bali ni kwa juhudi zake binafsi.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved