logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize: Napanga kumpa Kajala zawadi itakayompa kumbukumbu za milele, namheshimu!

Alipobanwa zaidi ikiwa zawadi hiyo itakuwa jaribio la kumtongoza kumrudia kwa mara ya 3 kama alivyofanya 2022 kwa kutumia Range Rover, Harmonize alisema itakuwa ni zawadi tu.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani08 April 2025 - 11:44

Muhtasari


  • Wawili hao wana historia ndefu ya mahusiano ya kifaurongo ambayo inarudi nyuma hadi mapema 2021 amapo walichumbiana kwa muda na kisha kuachana baada ya zogo lililohusisha binti ya Kajala, Paula, kuchangia.
  • Hata hivyo, mwaka mmoja baadae mnamo Juni 2022, Harmonize alijitutumua na kumrudisha Kajala kwenye kasri lake la Konde Village baada ya kumnunulia zawadi ya gari aina ya Range Rover 

Harmonize wakati alipompa Kajala zawadi ya Range Rover//Maktaba

BOSI wa Konde Music Worldwide, Harmonize kwa mara ya kwanza amezungumzia uhusiano wake na Kajala ambao ulivunjika – safari hii akizingatia upande wa mazuri yaliyotokana na uhusiano huo.

Akizungumza na blogu ya Simulizi na Sauti, Harmonize alibainisha kwamba bado anamheshimu Kajala Masanja kiasi kwamba anapangac kumpa zawadi nyingine ambayo aliitaja kuwa itampa kumbukumbu za milele katika kipindi chote cha maisha yake.

Alipobanwa zaidi ikiwa zawadi hiyo itakuwa jaribio la kumtongoza kumrudia kwa mara ya 3 kama alivyofanya 2022 kwa kutumia Range Rover, Harmonize alisema itakuwa ni zawadi tu bila kujali ikiwa atakuwa kwenye ndoa yake au la.

“Nina heshima kubwa sana kwa Kajala na kwa majaaliwa ya Mwenyezi Mungu, nitamfanyia kitu Fulani kwake ambacho kitakuwa na kumbukumbu ya milele maishani mwake. Haijalishi kama atakuwa ameolewa au la, atajua mwenyewe tu,” Harmonize alisema huku akiachia tabasamu pana.

Alipoulizwa kwa nini safari hii amelegeza msimamo wake kumhusu mama huyo wa binti mmoja mkubwa – kinyume na alivyomzomea kwenye wimbo wake wa Dear Ex, Harmonize alisema kwamba alijifunza kuanza kumheshimu ikizingatiwa kwamba ni mkubwa kwake kiumri.

“Kajala huwa namzungumzia kwa heshima kwa sababu ananizidi kiumri. Lakini pia ukiachia mbali kigezo hicho, nikiingia katika mahusiano naye kuna vitu vingi ambavyo nilimsababishia kwa hasara. Na siwezi lipa hilo kama mwanadamu hata kama sasa hatuko Pamoja ila bado anastahili heshima yake na hicho ndicho kitu ambacho ninampa,” Harmonize alisema.

Wawili hao wana historia ndefu ya mahusiano ya kifaurongo ambayo inarudi nyuma hadi mapema 2021 amapo walichumbiana kwa muda na kisha kuachana baada ya zogo lililohusisha binti ya Kajala, Paula, kuchangia.

Hata hivyo, mwaka mmoja baadae mnamo Juni 2022, Harmonize alijitutumua na kumrudisha Kajala kwenye kasri lake la Konde Village baada ya kumnunulia zawadi ya gari aina ya Range Rover na kuandaa tafrija kubwa la kumvisha pete ya uchumba Milimani City.

Penzi jipya lilidumu kwa miezi 6 tu kwani halikuweza kuona mwanga wa mwaka mpya wa 2023, safari hii wakiachana kimya kimya na siri za kuachana kwao zikafuatia baada ya miezi kadhaa, wote wakichambana kimafumbo kwenye mitandao ya kijamii.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved