logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize: Nina kila kitu nyumbani kwangu, kitu pekee ambacho sina ni hospitali tu!

Msanii huyo alitoa angalizo zaidi kwa yeyote ambaye angependa kujiunga naye kwenye mazoezi katika gym yake ya nyumbani, akisisitiza kwamba watoto wa kike tu ndio watakaokubaliwa.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 April 2025 - 14:27

Muhtasari


  • Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize alichapisha video akionyesha kukamilika kwa chumba chake cha mazoezi ya kunyanyua vyuma ambacho kimeshehedi vifaa vyote vya gym.
  • Harmonize alisema kwamba katika orofa ya juu, ana studio kwa ajili ya kufanya kazi zake za muziki na chini ana gym hivyo itakuwa vigumu sana kwa watu kukutana naye nje.

Harmonize

BOSI wa lebo ya muziki ya Konde Music Worldwide, Harmonize ameonyesha maendeoe ya jinsi anavyozidi kujiweka mbali na maisha ya nje, akisema kwamba lengo lake ni kuwa na kila huduma nyumbani kwake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize alichapisha video akionyesha kukamilika kwa chumba chake cha mazoezi ya kunyanyua vyuma ambacho kimeshehedi vifaa vyote vya gym.

Harmonize alisema kwamba katika orofa ya juu, ana studio kwa ajili ya kufanya kazi zake za muziki na chini ana gym hivyo itakuwa vigumu sana kwa watu kukutana naye nje.

Msanii huyo Alifichua kwamba itakuwa nadra sana kutangamana na watu nje ya jumba lake la Konde Village, akisema kwamba kitu pekee ambacho kitamfanya kutoka na anapoenda kutafuta matibabu kwani hospitali tu ndiyo hajaweka katika moja ya vyumba vyake.

Kwa mashabiki wake ambao wangependa kuchukua fursa muhali watakapomkuta, Harmonize aliwataka kufanya kumbukumbu njema naye ikitokea wamekutana nao nje, kwani kuonekana kwake kutakuwa kwa uchache wa ajabu.

“Itakuwa ghali sana kuniona pale nje, hebu tutengeneze kumbukumbu nzuri ikitokea tumekutana kwa maana sasa nina karibia kila kitu ndani. Kitu pekee ambacho pengine sina kwa sasa ni hospitali,” Harmonize aliandika.

Msanii huyo alitoa angalizo zaidi kwa yeyote ambaye angependa kujiunga naye kwenye mazoezi katika gym yake ya nyumbani, akisisitiza kwamba watoto wa kike tu ndio watakaokubaliwa.

“Nimerahisisha kila kitu, Konde Fitness iko tayari nyumbani kwangu, na ningependa kuwa na waalikwa lakini wawe warembo pekee. Mnaona gym iko chini na studio iko juu, juu ya dunia. Tag warembo wale ambao wanapenda kushiriki mazoezi ya gym waambie gym ya baba iko tayari,” Harmonize aliongeza.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved