logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Godlove ampa Stevo Sh1.9m na kusema “Nimemuunganisha na nguvu ya pesa na jicho la tatu!”

“Mimi narejesha baraka Zangu kwa kumbless kijana wao @stevosimpleboy8 million 40 za Tanzania 🇹🇿 kenya Ksh 1940000 nimemuunganisha na nguvu ya pesa na jicho la tatu.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani24 April 2025 - 11:59

Muhtasari


  • Kisha alichomoa Burunguti lingine na kumkabidhi akimwambia kwamba hizo zitawekwa pembeni hadi pale Simple Boy atakapotoa ngoma 3 nzuri.
  • Mwakibete aliahidi kwamba yeye ndiye atakayegharamia video za ngoma hizo 3 na kumtaka Simple Boy kuchakarika na kuhakikisha ni ngoma zenye mvuto na mnato.

Stevo Simple Boy apokea hela kutoka kwa Chief Godlove Mwakibete//Instagram

KIJANA mkwasi mwenye pesa zake kutoka Tanzania, Godlove Mwakibete maarufu kama Chief Godlove amempa msanii wa Kenya Stevo Simple Boy kitita cha hela ndefu kama zawadi.


Katika video aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram, Godlove alimkaribisha Stevo Simple Tanzania kwa Burunguti la hela noti za Tanzania na kumwambia kwamba hizo zitakuwa za matumizi yake wakati wa kipindi chake nchini humo.


Kisha alichomoa Burunguti lingine na kumkabidhi akimwambia kwamba hizo zitawekwa pembeni hadi pale Simple Boy atakapotoa ngoma 3 nzuri.


Mwakibete aliahidi kwamba yeye ndiye atakayegharamia video za ngoma hizo 3 na kumtaka Simple Boy kuchakarika na kuhakikisha ni ngoma zenye mvuto na mnato.


“Umekaribishwa Tanzania Stevo Simple Boy. Mimi sasa umefika kwangu na nataka ujue ukionana na Chief jua umeonana na pesa. Wakenya wanasema thamani ya hela za Tanzania iko chini kuliko za Kenya lakini hizi nakupa hapa ni za thamani kubwa ajabu,” Godlove alisema huku akifungua mkoba wake wa noti.


“Hizi zote ni kwa ajili ya matumizi yako ukiwa hapa Tanzania,” Godlove alimwambia huku akimkabidhi hela. “Hizi hapa zingine nitakuongeza pale ambapo utatoa hitsongs 3. Hizo ngoma 3 ni mimi nitagharamia video yazo. Nakulipia mimi mtoto mdogo mwenye hela nyingi. Na kuanzia leo wewe ni familia yangu,” Godlvoe aliongeza.


Stevo alisema hatolaza damu na atahakikisha ametoa ngoma hizo 3 ili kupata pesa hizo.

Stevo Simple Boy, Chief Godlove Mwakibete

Kwa upande wake Godlove, Alifichua kiasi cha hela hizo kwa jumla na kusema kwamba ndio rasmi amemtambulisha Stevo kwa nguvu ya pesa.


“Wakenya wananipenda sana na Mimi narejesha baraka Zangu kwa kumbless kijana wao @stevosimpleboy8 million 40 za Tanzania 🇹🇿 kenya Ksh 1940000 nimemuunganisha na nguvu ya pesa na jicho la tatu,” Godlove alikariri.


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved