logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Simple Boy: Mashabiki wakisema niache muziki nifanye ‘content creation’ siwezi pinga

“Mimi nafanya chenye mashabiki wanataka, wakisema content niko bora kuliko muziki ni poa lakini mimi kwangu nahisi muziki ndio niko bora,’ Simple aliongeza.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani06 March 2025 - 14:03

Muhtasari


  • Msanii huyo alikuwa akijibu swali la iwapo yeye ni mtengenezaji maudhui ya mitandaoni au ni mwanamuziki.
  • Hata hivyo, alisisitiza kwamba yeye hujihisi vizuri kufanya muziki ikilinganishwa na utengenezaji maudhui ya kuchekesha.

Stevo Simple Boy

MSANII kutoka Kibera, Stevo Simple Boy amefichua kwamba yeye yuko tayari kufanya chochote ambacho mashabiki wake watataka afanye, mradi tu awaburudishe.

Msanii huyo alikuwa akijibu swali la iwapo yeye ni mtengenezaji maudhui ya mitandaoni au ni mwanamuziki.

Simple Boy, ambaye anajulikana kwa mtindo wake wa rap na pia katika siku za hivi karibuni kwa kutengeneza maudhui kupitia Kauli na semi zake za ucheshi pamoja na uvaaji wake, alisema kwamba yuko tayari kufanya jinsi mashabiki watakavyotaka.

Hata hivyo, alisisitiza kwamba yeye hujihisi vizuri kufanya muziki ikilinganishwa na utengenezaji maudhui ya kuchekesha.

“Mwaka huu nimewapangia mashabiki muziki kibao, content na vitu vingine vingi. Mashabiki ndio wanasema kwamba mimi niko bora kwa content kuliko kwa muziki lakini mimi najua kwa muziki niko bora,’ Stevo alisema.

“Mimi nafanya chenye mashabiki wanataka, wakisema content niko bora kuliko muziki ni poa lakini mimi kwangu nahisi muziki ndio niko bora,’ Simple aliongeza.

Kuhusu suala la mapenzi, Simple Boy aliradidi kwamba kwa sasa yuko singo huku akisema kwamba mtoto aliyezaliwa na mpenzi wake wa awali si wake.

Alisema kwamba kwa sasa hafikirii kama atajitosa kwenye ulingo wa mapenzi tena, akidokeza kwamba mpenzi wake wa zamani alimsaliti.

“Mtoto si wangu, kwa sasa niko single na sitaki mahusiano ya mapenzi kwa sasa. Mimi niko sawa na mambo ya mapenzi nimeachana nayo kabisa kwa hiyo mashabiki zangu msitarajie shemeji yenu hivi karibuni,” alisema.

Kuhusu kurudiana na mpenzi wa kwanza, Pritty Vishy, Stevo alisisitiza kwamba hakuna jinsi watarudiana akitumia msmo maarufu kwamba ‘huwezi ukayarudia matapishi’.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved