logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize: Sijawahi enda kwa mganga katika maisha yangu, nategemea tu maombi ya babangu!

“Mimi sikumbuki kama nishawahi kwenda kwa mganga katika muda wangu wote kama ‘Harmonize’. Hii ni kwa sababu baba ananiombea sana, ananikumbusha vitu vya msingi,” Harmonize aliongeza.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani24 April 2025 - 10:45

Muhtasari


  • Akizungumza na Millard Ayo kwenye Ayo TV, Harmonize Alifichua kwamba hakumbuki hata siku moja akienda kutafuta huduma kwa mganga katika maisha yake ya muziki.
  • Alisema kwamba baba yake ni mtu wa dini sana na ndiye anayemuombea muda wote tangu ajitose kwenye muziki takribani miaka 10 iliyopita.

Harmonize//Screengrab-AyoTV-YouTube

MSANII Harmonize amekiri kwamba maombi ya babake ndiyo yanayompa mafanikio yake kimuziki licha ya kwamba baba huyo ndiye alikuwa anapinga sana suala la yeye kuwa mwanamuziki.

Akizungumza na Millard Ayo kwenye Ayo TV, Harmonize Alifichua kwamba hakumbuki hata siku moja akienda kutafuta huduma kwa mganga katika maisha yake ya muziki.

Alisema kwamba baba yake ni mtu wa dini sana na ndiye anayemuombea muda wote tangu ajitose kwenye muziki takribani miaka 10 iliyopita.

“Ninaweza sema hili, babangu mimi ni mtu wa dini sana. Hata wakati naanza muziki alikuwa ni mtu ambaye hakuwa kabisa na mimi. Lakini leo hii yeye ni kati ya watu ambao wananiombea sana,” Harmonize alisema.

“Mimi sikumbuki kama nishawahi kwenda kwa mganga katika muda wangu wote kama ‘Harmonize’. Hii ni kwa sababu baba ananiombea sana, ananikumbusha vitu vya msingi,” Harmonize aliongeza.

Msanii huyo alikuwa anazungumzia ufichuzi huu akirejelea kile alichokigusia kwenye wimbo wake wa ‘Never give up’ kwamba babake alikuwa mtu wa kuswali sana kiasi kwamba alinunia uamuzi wake wa kuingia kwenye sanaa.

“Acha nikuambie hadithi

Nimezaliwa mtwara Tanzania

Huko kijijini chitoholi

Hapa mjini nimezamia

Ndoto kucheza boli

Mara ghafla kwa mziki zikahamia

My dady im sorry swala tano Hukupenda uliposikia,” moja ya aya kwenye wimbo huo iliimba.

Harmonize pia alifunguka kuhusu picha na video zilizoenea akipokelewa kwao wakati alipotoka WCB Wasafi ambapo mbuzi alichinjwa na yeye kupakwa damu.

Alisisitiza kwamba ule haukuwa uchawi wala uganga wowote bali ilikuwa ni sehemu ya mila za kwao Mtwara ambayo babake alishauri ifanyike.

“Ile ilikuwa ni mila tu na wazazi wangu, haswa baba alishauri tufanye vile. Hivyo singeweza kukataa na wala hakuwahi kuniambia kwamba ule ni uchawi wa kumdhuru mtu au tumemwita mganga aje kufanya mambo yake.”

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved