logo

NOW ON AIR

Listen in Live

CS Murkomen Aomba IEBC Kupata Mwenyekiti Asiyetishika Kama Chebukati

“Naomba kwamba ile kamati ambayo inatafuta mwenyekiti wa IEBC ihakikishe kwamba imetafuta vile vigezo ambavyo vilikuwa kwa Chebukati.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari21 February 2025 - 14:15

Muhtasari


  • Kwa mujibu wa Murkomen, Chebukati alisimama kidete kutetea ukweli wa kikatiba bila kuyumbishwa, akisema kwamba hata IEBC ya sasa inafaa ipate mwenyekiti kama yeye.

Murkomen, Chebukati

WAZIRI wa masuala ya usalama wa ndani, Kipchumba Murkomen amemuomboleza aliyekuwa mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC, Wafula Chebukati kama mtu mkakamavu.

Murkomen alizungumza na vyombo vya habari saa chache baada ya taarifa kufichuka kwamba Chebukati amefariki.

Alimsifu Chebukati kama mtu ambayo aliacha alama ya kipekee katika kipindi chake cha miaka 6 kwenye tume hiyo.

“Wafula Chebukati atakumbukwa kwa uongozi wake wenye kanuni kanuni, ujasiri na uaminifu kwa Katiba. Akiwa mzalendo wa kweli na mtu mwadilifu sana, Chebukati aliongoza Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kupitia chaguzi mbili kitaaluma,” Murkomen aliandika kwenye X.

Pia alitoa wito kwa kamati itakayoongoza mchakato wa kuwachagua makamishna na mwenyekiti wa IEBC kuhakikisha kwamba tume hiyo inapata mwenyekiti mwenye misimamo ya kweli kama Chebukati.

Kwa mujibu wa Murkomen, Chebukati alisimama kidete kutetea ukweli wa kikatiba bila kuyumbishwa, akisema kwamba hata IEBC ya sasa inafaa ipate mwenyekiti kama yeye.

“Naomba kwamba ile kamati ambayo inatafuta mwenyekiti wa IEBC ihakikishe kwamba imetafuta vile vigezo ambavyo vilikuwa kwa Chebukati. Kwa sababu tunataka mtu ambaye hawezi akatishwa.”

“Mtu ambaye hawezi tishwa na upande wa serikali na hawezi tishwa na upande wa upinzani kwa sababu yeye ni refa lazima asimamie upanjde wa katiba, na ukisimama upande wa katiba huwezi kosea,” Murkomen aliongeza.

Alisema kwamba IEBC inastahili mtu ambaye anasimamia ukweli na kusikiliza ushauri wa kweli bila kutegemea maoni yake binafsi kufanya maamuzi.

“Asikuwe ni mtu ambaye anafuata maoni yake binafsi, mtu ambaye hana uzalendo, mtu ambaye hazingatii mambo ya taifa, unajua kwamba sisi wenye tunasimamia mambo ya usalama, tishio kubwa ni wale ambao wanatenda mambo ya kuwakera wananchi. Kwa hivyo tunataka mtu mwenye atachaguliwa awe ni mwenye atasimamia katiba,” Murkomen alisema.

×

Chebukati alitangazwa kufariki mapema Ijumaa ya Februari 21 baada ya kuugua kwa muda katika hospitali moja jijini Nairobi.

Alifariki akiwa na umri wa miaka 64 na alihudumu kama mwenyekiti wa IEBC kwa miaka 6, Januari 2017 hadi Januari 2023.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved