logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Hatua Ya Raila Kuwania AUC Iliwaunganisha Wakenya Wote Pamoja!” – Rais Ruto

“Uwaniaji wake uliwaleta pamoja Wakenya wote. Nafikiri uwaniaji wake ulivutia sapoti kutoka kwa mirengo yote ya kisiasa – watu kutoka serikali, upinzani na kila mtu.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari24 February 2025 - 14:18

Muhtasari


  • Mkuu wa taifa alichukua fursa hiyo kuwashukuru wote waliochangia kwa njia kubwa ama ndogo katika kutangaza azma ya Odinga katika kinyang’anyiro cha AUC.
  • Rais pia aliwashukuru wakuu wa mataifa 22 ambao walisimama imara ya mwaniaji wa Kenya katika raundi zote hadi alipojiondoa kunako raundi ya 6.

Ruto na Raila

RAIS William Ruto amedai kwamba hatua ya kiongozi wa ODM, Raila Odinga kuwania uenyekiti wa AUC, japo bila mafanikio, iliwaunganisha Wakenya wote pamoja.

Akizungumza katika ikulu ya Mombasa alikomkaribisha Odinga aliyerejea nchini baada ya kupoteza kinyang’anyiro cha AUC wiki iliyopita, Ruto alimshukuru kwa kuliwakilisha taifa katika ngazi za kimataifa.

“Ninajivunia kwamba Raila Odinga aliweka juhudi zote kuwa mwaniaji mwenye nguvu barani Afrika. Alifanya safari angani na barabarani akizuru mataifa mbalimbali kujipigia debe si tu kwa niaba yake bali pia kwa niaba ya Kenya,’ Ruto alisema.

“Uwaniaji wake uliwaleta pamoja Wakenya wote. Nafikiri uwaniaji wake ulivutia sapoti kutoka kwa mirengo yote ya kisiasa – watu kutoka serikali, upinzani na kila mtu. Tuliungana nyuma ya uwaniaji wa Raila Odinga kama mwenyekiti wa AUC,” rais aliongeza.

Mkuu wa taifa alichukua fursa hiyo kuwashukuru wote waliochangia kwa njia kubwa ama ndogo katika kutangaza azma ya Odinga katika kinyang’anyiro cha AUC.

Rais pia aliwashukuru wakuu wa mataifa 22 ambao walisimama imara ya mwaniaji wa Kenya katika raundi zote hadi alipojiondoa kunako raundi ya 6.

“Ningependa kuwashukuru ndugu zangu na marafiki zangu kote barani Afrika kwa ishara yao ya mshikamano na sapoti ambayo walionyesha kwa Kenya na kwa Raila Odinga ambaye alikuwa mgombea wetu.”

Raila Odinga alijiondoa katika raundi ya 6 baada ya kupata kura 22 dhidi ya kura 26 alizopata mshindani wake kutoka Djibout, Youssouf Mahmoud Ali.Youssouf hatimaye aliibuka mshindi katika raundi ya 7 ambapo alipata akidi hitajika ya kura 33 na kuchukua uongozi kutoka kwa Moussa Faki aliyekuwa anamaliza hatamu yake.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved