logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Msaliti ni nani? Hakuna mtu tumesaliti” – Raila atetea kuungana na rais Ruto

“Msaliti ni nani? Hakuna mtu tumesaliti. Sisi tuliandika mambo 10 muhimu zaidi, tukasema haya mambo yakirekebishwa tuko tayari kufanya kazi sawa sawa,” Odinga alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari10 March 2025 - 15:02

Muhtasari


  • Alisisitiza kwamba yeye si msaliti kama ambavyo sehemu ya Wakenya walihisi baada ya kutia Saini mkataba wa makubaliano ya kufanya kazi Pamoja kati ya ODM na UDA.
  • “Msaliti ni nani? Hakuna mtu tumesaliti. Sisi tuliandika mambo 10 muhimu zaidi, tukasema haya mambo yakirekebishwa tuko tayari kufanya kazi sawa sawa,.

Raila Odinga na William Ruto baada ya kusaini mkataba wa ushirikiano baina ya ODM na UDA

KINARA wa chama cha ODM, Raila Odinga amesisitiza kwamba hakuna Mkenya yeyote ambaye alisaliti wakati aliamua kushikana na rais William Ruto mwishoni mwa juma lililopita.

Akizungumza katika hafla ya mazishi katika Kijiji cha Nyaduong’, Wadi ya God Jope, Eneobunge la Suna Mashariki, Kaunti ya Migori Jumapili, Odinga alisema kwamba kushikana kwa ODM na UDA ni kwa maslahi ya wananchi wanaotaka maendeleo.

Alisisitiza kwamba yeye si msaliti kama ambavyo sehemu ya Wakenya walihisi baada ya kutia Saini mkataba wa makubaliano ya kufanya kazi Pamoja kati ya ODM na UDA.

“Msaliti ni nani? Hakuna mtu tumesaliti. Sisi tuliandika mambo 10 muhimu zaidi, tukasema haya mambo yakirekebishwa tuko tayari kufanya kazi sawa sawa,” Odinga alisema.

Ni kauli ambayo ilisisitizwa na rais Ruto ambaye alikuwa katika ibada ya kanisa kaunti ya Uasin Gishu, akisema kwamba makubaliano ya oni ya kuhakikisha hakuna eneo la nchi ambalo litasalia nyuma kimaendeleo.

“Hakuna jamii au eneo la Kenya ambalo litasalia nyuma kimaendeleo,” Ruto alisema.

Hata hivyo, sehemu ya Wakenya wanaendelea kuhisi kwamba Odinga hakufaa kuungana na rais Ruto na kutoridhishwa huku kulishuhudiwa katika kaunti ya Kisii wakati wakaazi waliondoka kwa manung’uniko mengi baada ya Odinga kuwasili.

Mashabiki wengi waliokuwa wakijumuika katika uwanja wa Gusii kwa hafla ya uzinduzi wa jezi mpya za klabu ya Shabana FC waliondoka kwa ghadhabu wakionesha kutoridhishwa kwao na hatua ya Odinga kuungana na rais Ruto.

Mwishoni mwa juma lililopita, viongozi hao wawili walitia Saini mkataba wa makubaliano ya kufanya kazi Pamoja huku wakisisitiza jumla ya masuala 10 ambayo yatafanikishwa na ukuruba huu mpya.

Yafuatayo ni mambo hayo makuu ya mkataba wa UDA-ODM:

1. Utekelezaji kamili wa ripoti ya Nadco (Kamati ya Mazungumzo ya Kitaifa).

2. Ushirikishwaji katika mgao wa bajeti na uteuzi wa umma

3. Kulinda na kuimarisha ugatuzi

4. Uwekezaji wa kiuchumi kwa vijana

5. Uongozi, uadilifu & mwisho wa kuonyesha utajiri

6. Haki ya kukusanyika kwa amani, fidia ya madai yote yanayosubiri ya waathiriwa wa haki

7. Ukaguzi wa deni la Taifa na jinsi lilivyotumika

8. Kupambana na rushwa

9. Kukomesha ufujaji wa rasilimali za umma

10. Kulinda uhuru wa watu, kukomesha utekaji, kuheshimu katiba na utawala wa sheria na kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved