logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Maisha yangu yamo hatarini!” Gachagua amlilia Inspekta Jenerali wa Polisi

Gachagua amekuwa mkosoaji mkuu wa serikali ambayo kwa kipindi kimoja alikuwa anaitetea kwa jino na ukucha hadi pale alipobanduliwa ofisini mnamo Oktoba 2024.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari15 April 2025 - 09:51

Muhtasari


  • Gachagua amekuwa mkosoaji mkuu wa serikali ambayo kwa kipindi kimoja alikuwa anaitetea kwa jino na ukucha hadi pale alipobanduliwa ofisini mnamo Oktoba 2024.
  • Gachagua alitolea mifano mashambulizi ambayo alidai yamekuwa yakilenga mikutano yake ya kisiasa na kudai kwamba ipo njama fiche ya kulenga maisha yake.

Rigathi Gachagua

NAIBU wa rais aliyebanduliwa, Rigathi Gachagua amelilia vyombo vya usalama akisema maisha yake yamo hatarini.

Kupitia taarifa rasmi aliyoichapisha kwenye kurasa zake katika mitandao ya kijamii, Gachagua aliandikia wakuu wa vitengo mbalimbali vya usalama akiwemo IG wa polisi Douglas Kanja, na kudai kwamba amepokea vitisho kuhusu maisha yake.

Gachagua alitolea mifano mashambulizi ambayo alidai yamekuwa yakilenga mikutano yake ya kisiasa na kudai kwamba ipo njama fiche ya kulenga maisha yake.

“Kama unavyojua, una wajibu wa kikatiba kulinda kila mkenya na mali zao kama ilivyoainishwa katika katiba ya 2010. Hata hivyo, katika kesi hii, bwana Kanja unaendeleza mashambulizi na uhalifu,” sehemu ya barua hiyo iliyoelekezwa kwa ofisi ya IG Kanja ilisoma.

Aidha, Gachagua alilalamikia kuondolewa kwa walinzi wake akisema kwamba suala hilo limemuanika bayana kwa mashambulizi ambayo sasa yameweka maisha yake hatarini.

“Uliondoa walinzi wangu katika njama iliyopangwa vizuri ili kunianika zaidi kwa visa vya kushambuliwa na vijana kwa kushirikiana na vyombo vya usalama,” alilalama zaidi akitolea mifano ya mashambulizi dhidi yake katika hafla mbalimbali za umma.

Kisa cha hivi punde cha mashambulizi dhidi ya naibu wa rais huyo wa zamani kilijiri wiki mbili zilizopita katika hafla ya ibada kanisani PCEA Mwiki.

Iliwabidi walinzi wake wa Kibinafsi kuingilia kati na kufyatua risasi hewani ili kutawanya kundi la vijana ambao walifika katika kanisa hilo wakipiga kelele kuhusu Gachagua.

Gachagua amekuwa mkosoaji mkuu wa serikali ambayo kwa kipindi kimoja alikuwa anaitetea kwa jino na ukucha hadi pale alipobanduliwa ofisini mnamo Oktoba 2024.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved