logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kamagut: Watoto wafukua maiti ya baba aliyezikwa 2010 wakimtaka atatue mzozo wa shamba

Hata hivyo, polisi walifika katika boma hilo na kuwatia mbaroni vijana hao 3 pamoja na mama yao mjane kwa kile walisema kwamba ni kuzua usumbufu kwa marehemu.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Mahakama07 April 2025 - 11:17

Muhtasari


  • Walieleza kuwa walitoa taarifa za vitisho hivyo kwa mamlaka, lakini bila msaada wowote, walimgeukia mtu huyo ambaye alikuwa akiwalinda wakati wote akiwa hai.
  • Mtoto mmoja wa marehemu, alisema unyanyasaji huo uliongezeka siku ya Jumamosi wakati vijana waliokuwa na mapanga walipovamia shamba hilo na kuanza kupanda mazao sehemu moja.

Jeneza la marehemu//Maktaba

WAKAAZI wa Kijiji cha Kamagut katika kaunti ya Uasin Gishu walipigwa na butwaa wikendi iliyopita baada ya vijana wa boma moja kufukua mwili wa marehemu baba yao aliyezikwa miaka 15 iliyopita wakimtaka aingilie kati mzozo wa shamba.

Kwa mujibu wa The Standard, mwili wa mzee huyo ulikuwa umefukuliwa na watoto wake, ambao walidai ni yeye pekee anayeweza kuwatetea dhidi ya vitisho vya mara kwa mara na mtu anayedai umiliki wa shamba lao la ekari 17, linalodaiwa kurithi kutoka kwa nyanya yao.

Ripoti hiyo ilieleza kwamba Watoto wa mzee huyo walifikia uamuzi huo baada ya majambazi kuendelea kuwatishia kuwaondoa kwenye mali hiyo tangu mwaka 2022.

Walieleza kuwa walitoa taarifa za vitisho hivyo kwa mamlaka, lakini bila msaada wowote, walimgeukia mtu huyo ambaye alikuwa akiwalinda wakati wote akiwa hai.

Mtoto mmoja wa marehemu, alisema unyanyasaji huo uliongezeka siku ya Jumamosi wakati vijana waliokuwa na mapanga walipovamia shamba hilo na kuanza kupanda mazao sehemu moja.

Alisema yeye na ndugu zake kwa heshima waliwaomba wavamizi hao kuondoka kwenye mali hiyo, lakini walishambuliwa kwa mapanga na visu.

Hata hivyo, polisi walifika katika boma hilo na kuwatia mbaroni vijana hao 3 pamoja na mama yao mjane kwa kile walisema kwamba ni kuzua usumbufu kwa marehemu.

Kamanda wa polisi kaunti ya Uasin Gishu Benjamin Mwanthi alithibitisha kwa The Standard kuwa wanne hao walikamatwa kwa kufukua mwili bila agizo la mahakama.

"Ni kinyume cha sheria kufukua maiti iliyozikwa-hata ikiwa ni ya jamaa-bila idhini inayofaa. Pia ni kinyume cha sheria kuingilia mabaki ya binadamu," alisema Kamanda wa Kaunti.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved