logo

NOW ON AIR

Listen in Live

‘Wazazi Wangu Wamenikasirikia Sababu Mume Wangu Hakuwatumia Pesa Krisimasi’

Kwa mujibu wa Lavender, wazazi wake walimpigia simu Desemba 24 na kumuomba pesa za Krismasi ambapo aliwaahidi kuwaombea kwa mumewe ‘hustler’ lakini hakufanikiwa kutuma.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Vipindi21 February 2025 - 09:00

Muhtasari


  • Baadae Desemba 26, wazazi walimpigia tena wakitaka kujua nini kilitokea hawakutuma ambapo Lavender aliahidi kufanya hivyo Januari mosi lakini pia hawakufanikiwa.
  • Hapo ndipo wazazi na ndugu zake waliamua kumblock kwa pamoja wakidai kwamba hawasaidii licha ya kumsomesha na baadae akaoleka.

Gidi na Ghost

MREMBO mwenye umri wa miaka 25, Mercy Lavender kutoka jiji la Nakuru ni mtu mwenye mawazo mengi baada ya wazazi wake kumkasirikia kwa sababu ya kutowatumia pesa za kusherehekea Krismasi.

Lavender alipeleka masaibu yake katika kipindi cha Patanisho kwenye Gidi na Ghost katika Radio Jambo na kusimulia jinsi wazazi wake walikata uhusiano naye baada ya tukio hilo la Desemba mwaka jana.

Kwa mujibu wa Lavender, wazazi wake walimpigia simu Desemba 24 na kumuomba pesa za Krismasi ambapo aliwaahidi kuwaombea kwa mumewe ‘hustler’ lakini hakufanikiwa kutuma.

Baadae Desemba 26, wazazi walimpigia tena wakitaka kujua nini kilitokea hawakutuma ambapo Lavender aliahidi kufanya hivyo Januari mosi lakini pia hawakufanikiwa.

Hapo ndipo wazazi na ndugu zake waliamua kumblock kwa pamoja wakidai kwamba hawasaidii licha ya kumsomesha na baadae akaoleka.

“Nilikosana na wazazi wangu Desemba, 24 babangu alinipigia akiniomba sikukuu nikamwambia ni sawa lakini mimi sina kazi, Desemba 25-26 kufika, baba akapiga simu akaniambia nimepanga aje nikamwambia mzee wangu amesema atatuma Januari mosi,” alisema.

“Baada ya hapo ikabidi ameambia dada zangu waliblock akisema walinisomesha nikaoleka na siwasaidii,. Wakaniblock wote mpaka mama hawakati stori zangu eti mimi siwapi kitu tangu nioleke na mimi sina kazi na mzee wangu ni hustler….”

Mercy alisema kwamba kinachomsumbua sana ni laana ambazo wamekuwa wakimtamkia na angependa kuzungumza na babake ili arudishe hayo maneno ya laana.

“Sasa wamekuwa wakinirushia laana nyingi sasa nikakaa nikasema wacha nipatanishwe na babangu kwa sababu kusema ukwli mimi mwenyewe sina pesa na wamekuwa wakinirushia laana,” Mercy alisema.

Kwa upande wake mzee alipopigiwa simu, alisema kwamba ni kweli walimkasirikia binti yake kwa sababu alikuwa amemsaidia pesa kidogo akisema kwamba hawakukosana bali alitaka tu kunyamaza ili kumzuia asimuombe pesa tena.

“Mimi niliona tu ninyamaze lakini sikumwambia asikuje nyumbani. Niliwasaidia tu hadi nikaona ninyamaze wenyewe waone vile watafanya,” mzee alisema.

Bintiye alizungumza naye akimuomba msamaha na kusema kwamba ni vile yeye na mumewe hawana kitu na siku watakuja kupata watamsaidia.

Mzee pia aliahidi kwamba atam’unblock binti yake na kumtaka kuacha kumpeleka mama yake mbio kwa simu.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved