logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Naomba mke wangu anisamehe kwa kutaka kujua watu wanaompigia simu

Steven alieleza kwamba anahisi kabisa yeye ndiye alimkosea mkewe kwa hulka yake ya kukurupukia simu yake kila mara ilipokuwa inapigwa.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Patanisho17 March 2025 - 08:57

Muhtasari


  • Steven alieleza kwamba anahisi kabisa yeye ndiye alimkosea mkewe kwa hulka yake ya kukurupukia simu yake kila mara ilipokuwa inapigwa.
  • Betty Wanyonyi kwa upande wake alithibitisha kwamba ni kweli tabia ya mumewe kurukia simu yake ndiyo iliyomfanya kuchukua uhusiano wao na kutaka kuivunja.

Katika kipindi cha Patanisho kwenye stesheni ya Radio Jambo, jamaa kwa jina Steven kutoka Kitale aliomba kupatanishwa na mkewe ambaye walikosana baada ya kukaa kwenye ndoa ya miaka 3.

Gidi na Ghost kwenye Patanisho

Steven alieleza kwamba anahisi kabisa yeye ndiye alimkosea mkewe kwa hulka yake ya kukurupukia simu yake kila mara ilipokuwa inapigwa.

Alisema kwamba kila mara simu ya mkewe ilipokuwa inapigwa, alikuwa anataka kujua ni nani huyo aliyekuwa anampigia, jambo ambalo lilionekana kumkasirisha mkewe.

“Tulikuwa tunaishi kwa ndoa miaka 20, tulianza kuchumbiana 2021 tukakuwa tukivurugana tu mambo ya simu. Mtu akimpigia nilikuwa nataka kujua ni nani anampigia na kwa kweli mimi ndiye nilikuwa mwenye makosa. Hilo ni kama lilimkasirisha. Alitoka yuko mahali anafanya kazi na huwa tunaongea lakini nahisi nilimkosea nataka ajue kwamba bado nampenda,” Steve alisema.

Betty Wanyonyi kwa upande wake alithibitisha kwamba ni kweli tabia ya mumewe kurukia simu yake ndiyo iliyomfanya kuchukua uhusiano wao na kutaka kuivunja.

“Mimi ni yule ninauza kwa duka, mteja akipiga simu kuulizia kuhusu bidhaa huyo mume wangu anaanza kuhisi kwamba ninamsaliti katika mapenzi. Kila wakati mwenye anapigac simu anataka kuona ni nani na hicho ndicho kilinifanya nikakasirika.

“Hata kama kuna wale wateja ambao wanajaribu kunitongoza nilikuwa nawaambia kwamba nimeolewa,” Betty alijieleza.

 “Nataka tu kukuomba msamaha na hata hayo mambo ya simu sitawahi shika simu yako hata siku moja,” Steven alinyenyekea akisisitiza kuikwepa kabisa simu ya mpenziwe.

Baada ya tathmini ya muda, Betty alitamka kwamba amemsamehe huku Steven akieleza furaha yake baada ya kusamehewa na mpenzi wake.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved