- Wanamitandao wawashambulia wanawake waliokuwa na Eric Omondi
Licha ya hali ngumu ambayo inashuudiwa nchini kote na wengi kutopata pesaza kukimu maisha yao mchekeshaji Eric Omondi alionekana kufurahia maisha yake baada ya kutafuta mwanamke wa kuoa huku akiwapata wanawake tisa ambao walifanya mitihani kadha wa kadha.
Wanawake hao walionekana wakijikakamua kila upande ili wachaguliwe na mashabiki nani ameitimu kuwa mkewe mchekeshaji huyo.
Baada ya Eric Omondi kupakia video akiwa na wanawake hao kwa siku ya mwisho huku wakingoja kupigiwa kura siku ya jumatano wiki ijayo wanamitandao hawakulaza damu mbali waliwasuta wanawake hao.
Kuna wale walibaki na swali je wanwake hao wataolewa na nani.
Huku wengine walijitokeza na kusema kwamba siku hizi au karne hii ya sasa wanawake hawaaminiki na hawana dhamana kwa ajili ya tabia zao.
Pia wengine walisema kwamba wanawake wa siku hizi hawana haja na uhusiano wowote au mapenzi bali wanapomuona mwanamme akiwa na pesa wanajipendekeza.
Hizi hapa baadhi za hisia za wanamitandao;
mercy_ramsey: Kweli wanawake siku hizi hawana dhamana cheap sana
paulinekemmy1 :Enyewe we are cheap more especially when we see money
kimutai_gregzi :wonder who will proudly say I want to marry such type of women๐
vehuhar: I think this stupidity should be banned frm social media. These girls are so awkward and lowering their dignity
vivienewendy :Surely sasa hao wasichana do they have parents?
massawejapanni: My goodness! Her spine!!!.Kisa show?๐๐๐ !!!!
khadhija_mswahili :Nauliza Hawa wanawake shida ni nini.kujianika yote hii kisa kuolewa nkt.
malimachristopher: Hao hawana thamani kabisa mtu anawafanyia comedy mkiwa uchi anawabadilisha apendavyo
djshiti_comedian :Wasanii tuwache mihadarati๐ ๐