'Uchawi kila mahali,'Akothee aapa kutoa uhusiano wake wa kimapenzi mitandaoni

Muhtasari
  • Akothee aapa kutoa uhusiano wake wa kimapenzi mitandaoni
Image: INSTAGRAM// AKOTHEE

Baada ya Corazon Kwamboka kutangaza kwamba ametengana na baba ya watoto wake wengi waliachwa vinywa wazi huku wanamitandao wakitoa hisia tofauti.

Kufuataia kutengana kwao msanii maarufu nchini Akothee ameapa kutoa uhusiano wake mitandaoni.

Mama wa watoto watano aliomboleza jinsi uhusiano wa watu mashuhuri unavyoisha haraka kuliko mtu anavyoweza kupepesa macho.

"We! Kiwango cha kesi za talaka na kuachana kimekwisha, ngoja nikae tu nile ice cream. Sasa uhusiano gani unafanya kazi? nikifungua mitandao naona talaka kila mahali.

Lakini haikuwa hivyo tu, aliongeza kuwa licha ya mifarakano kati ya watu mashuhuri bado alikuwa akiwaona wanandoa wenye furaha.

Lakini hilo halikuonekana kumfurahisha Akothee na kutangaza kwamba ataacha kuweka maisha yake ya mapenzi kwenye mitandao ya kijamii.

"Nikifungua mitandao naona wanandoa wenye furaha kila mahali! Ahhh! Acha niondoe maisha yangu ya mapenzi kwenye mitandao ya kijamii. Ahhh, ahhhh, ahhhh ni mbaya."

Kisha akamaliza kwa kusema kuna watu wengi huko nje ambao wanataka kuona mabaya zaidi kwa mtu.

Alibainisha kuwa watu hao watasherehekea wakati uhusiano wa mtu unapopungua, kwa kutumia nyakati za furaha zilizopita kuwachukia.

"Wachawi, uchawi kila mahali. Mitandao haitakupa hata wakati wa kupona au kujua kitu kabla ya kukuletea nyakati zote za kupendeza usoni pako."