Thicky Sandra amefichua ni nini kingehitajika kwa mtu kumuoa

Bintiye mwanasiasa Mike Sonko, Sandra Mbuvi, almaarufu Thicky Sandra, amefichua ni nini kingehitajika kwa mtu kumuoa.

Muhtasari
  • Alikuwa akimjibu shabiki aliyeuliza mahari yake ingegharimu kiasi gani.

Bintiye mwanasiasa Mike Sonko, Sandra Mbuvi, almaarufu Thicky Sandra, amefichua ni nini kingehitajika kwa mtu kumuoa.

Wakati wa kipindi cha Maswali na majibu na mashabiki wake kwenye Instagram, Sandra alishiriki mahari yake ya matarajio.

Alikuwa akimjibu shabiki aliyeuliza mahari yake ingegharimu kiasi gani.

"Mahari yako ni kiasi gani mpenzi wangu?" shabiki aliuliza.

"Wazazi wangu wanataka simba watano, chopper tatu, Bentley 22, rover nne na pauni milioni 500," Sandra alijibu.

Jibu lake lilizua hisia nyingi mtandaoni huku wengine wakishangaa hizo zote ni za nini na wengine wakiungana na yeye kwa kuwa ni mrembo.

mtayarishaji wa maudhui vincet mboya alimtumia ujumbe akidai kuwa anaweza kulipia mahari yake lakini mwanadada huyo alimkataa.

mazungumzo kati ya vincent mboya na Thicky sandra
Image: Instagram//NGC

Pia alizungumza kuhusu maisha yake ya mapenzi wakati shabiki alipomuuliza kama yuko kwenye uhusiano wakati wa sehemu ya maswali na majibu.

"Uko na mtu?" aliulizwa.

"Mahusiano yanapunguza kasi yangu, yanapunguza maono yangu,"  Sandra alisema.

Kisha akafichua kuwa mpenzi wake anayefaa anapaswa kuwa na urefu wa angalau futi 6.

Shabiki mmoja alipoona fursa ya kupiga shuti lake, alionyesha nia ya kumfungulia yaliyokuwa moyoni na kumuuliza ikiwa angeithamini.

Walakini, majibu yake hayakuwa ya kishenzi.

"Nikikupa moyo wangu, utauhifadhi milele?" Aliuliza.

"Hapana," Sandra alijibu.

Pia aliulizwa  anavyochanganya shule na kazi, Sandra alifichua kwamba hafanyi hivyo peke yake na kuna watu amao wanamsaidia.

"Unawezaje kuchanganya shule na biashara zako?" shabiki aliuliza.

"Nina wasimamizi," alijibu.