logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vera Sidika: Kusafiri Nje ya Nchi Mara 1 Kwa Mwezi Kunaweka Daktari Mbali Nami

Wengine walijisikitikia kwamba hana kaunti za Kenya 47 hawajawahi zizuru zote wakati Sidika tayari analeta wazo la kusafiri kimataifa angalau mara moja kwa mwezi.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani27 February 2025 - 16:10

Muhtasari


  • Kwa mujibu wa Sidika, anatarajia kufanya ziara moja ya kimataifa nje ya Kenya angalau mara moja kwa mwezi, akifichua tayari mwezi Februari amekamilisha safari 2 kimataifa.
  • Watu katika kutoa maoni walimshabiki kwa kile walidai kwamba yeye ndiye mwanasosholaiti asiyeogopa kumtumia esa kujivinjari.

Vera Sidika
MWANASOSHOLAITI Vera Sidka amefichua jinsi anakuwa makini na afya yake ikiwemo tiba asili ambayo kwa muda mrefu imemuacha akiwac na afya bila kulazwa wala kuona daktari.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Sidika alichapisha picha akiwa amestarehe kwenye ndege na kufichua kuwa ndio alikuwa anarudi nchini Kenya baada ya ziara ya siku kadhaa nchini Marekani.


Kwa mujibu wa Sidika, anatarajia kufanya ziara moja ya kimataifa nje ya Kenya angalau mara moja kwa mwezi, akifichua tayari mwezi Februari amekamilisha safari 2 kimataifa.


Mama huyo wa watoto wawili aliwapa ushauri wa bila malipo mashabiki na wafuasi wake akiwaasa kwamba ikiwa wangependa kuishi maisha ya afya bila kulazimika kuonana na daktari mara kwa mara, basi wafanye kuwa kawaida kwao kusafiri nje ya nchi angalau mara moja kwa mwezi.


“Narejea kwenye uhalisia …Narudi Kenya 🇰🇪✈️ Kwa kweli nilipata msisimko 💥 hakika safari 1 ya kimataifa kwa mwezi huwaweka madaktari mbali! Ni Mwezi wa 2; na tayari nimekamilisha ziara kwa nchi 2. Siwezi kusubiri matukio ya Machi,” Sidika alikariri.


Watu katika kutoa maoni walimshabiki kwa kile walidai kwamba yeye ndiye mwanasosholaiti asiyeogopa kumtumia esa kujivinjari.


Wengine walijisikitikia kwamba hana kaunti za Kenya 47 hawajawahi zizuru zote wakati Sidika tayari analeta wazo la kusafiri kimataifa angalau mara moja kwa mwezi.


@simba.tito: “Mimi mwenyewe 47 counties sijamaliza.”


@bellah_ayuma: “God, please, futa hio yenye nlikua nmesema when I grow up, I want to be Amberray futa ueke Vera please.”


@doriceliyoko: “Ukianza kucatch flights hutaki kamwe kuacha aki. Ni kama dawa.”

Ungamo la Sidika kuhusu kuwa na uraibu wa kusafiri kimataifa angalau mara moja kwa mwezi linajiri wakati ambapo nchini kumekuwa na vita vya maneno baina ya mwanasosholaiti Amber Ray na baadhi ya watumizi wa mitandao ya kijamii.

Mgogoro huo ulianza pale ambapo baadhi walimsuta Amber Ray wakimtaka kukoma kujitambua kama 'bibi ya tajiri' wakati hajawahi fanya ziara ya nje ya nchi.

Hata hivyo, Amber Ray alijitetea akionesha risiti za ziara zake za nje ya nchi, risiti ambazo zilichambuliwa vikali na kudhihakiwa.

 


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved