logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanaume Waluhya ni kama tu Wanigeria, wanapenda viuno pana! – Vera Sidika

Alisema kwamba wanaume wa Kenya wengi wao wanapenda wanawake wenye wako na ‘curves’ lakini pia akasema ndio wanajua ku’treat wanawake curvy vizuri.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani24 March 2025 - 15:13

Muhtasari


  • Alisema kwamba wanaume wa Kenya wengi wao wanapenda wanawake wenye wako na ‘curves’ lakini pia akasema ndio wanajua ku’treat wanawake curvy vizuri.
  • “Wanaume wa Kenya huwa wanapenda curves lakini ninafikiria ni nani atakuweza…. Lakini nahisi wanaume Waluhya – jamii yangu hiyo – wanakuweza sana.”

Vera Sidika

VERA Sidika ametetea wanaume kutoka jamii yake ya Abaluhya akisema kuwa hao ndio wanaopenda wanawake wenye viuno vipana.

Akizungumza na mwanablogu Afolasade Samagbeyi kupitia kwa podkasti yake, Sosholaiti huyo alisema kuwa wanaume Waluhya si tu wanapenda wanawake waliobarikiwa na upana wa viuno lakini pia wanajua jinsi ya kuwadekeza.

Sidika alikuwa anajibu swali la Samagbeyi aliyetania kwamba angependa kuolewa na mwanamume wa Kenya lakini akawa hajui ni wanaume wepi wa Kenya ambao wanaweza kumpenda jinsi alivyo.

Vera Sidika akirejelea umbo la kiuno kipana cha Samagbeyi, alisema kwamba wanaume wa Kenya wengi wao wanapenda wanawake wenye wako na ‘curves’ lakini akawapigia upato zaidi wanaume Waluhya akisema ndio wanajua ku’treat wanawake curvy vizuri.

“Wanaume wa Kenya huwa wanapenda curves lakini ninafikiria ni nani atakuweza…. Lakini nahisi wanaume Waluhya – jamii yangu hiyo – wanakuweza sana.”

“Nahisi Waluhya wako zaidi kama Wanigeria., unajua wana miili yenye nguvu na wanavutia na unajua wako na vibes nzuri na pia wanajua kudekeza. Utapenda na utakuwa unapika ugali…kwa kweli siwezi ngoja,” Sidika alimtania Samagbeyi.

Hii si mara ya kwanza kwa mama huyo wa watoto wawili kufichua waziwazi mapenzi yake kwa wanaume Wanigeria.

Mwezi Mei mwaka jana, Sidika alifichua kwamba alikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na mwanaume kutoka Nigeria, japo akasisitiza kwamba huba lao si la kuelekea katika ndoa bali ni kujivinjari tu.

"Kwangu mimi, sitaki kujitolea chochote kwa sasa. Nataka tu kufurahia – niko na mtu lakini sitasema niko kwenye uhusiano wa dhati. Ni kama sijajitolea kwa sababu sikutaka iwe serious...niko 50/50 mguu mmoja ndani, mguu mmoja nje.”

"Sitaki ajitume na sitaki kujitolea. Yeye ni Mnigeria. Unajua jinsi wanavyosema ukiwa mweusi haurudi nyuma, ni kama ukienda Nigeria haurudi nyuma. Ilikuwa kama nilipotea mahali fulani na sasa nimerudi kwa mtu sahihi,” alisema.

Vera alizidi kusema kuwa; "Wanaume wa Nigeria wanapenda wanawake walio na viuno pana…Wanaume wa Nigeria ni wanaume sana na hawaogopi mtu yeyote, hawaogopi kukuambia unapokosea na ninahitaji hilo.”

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved