logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pasta atabiri ndoa nyingi kuvunjika mwezi Aprili, ‘Wanaume watapoteza nguvu za kiume!’

“Aprili 2025 ukimuona mumeo hana nguvu za kiume, tulia hapo hapo. Hapo utakapotaka kukimbilia penyewe pia hazitakuwepo. Muombee mumeo!” pasta alishauri.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani28 March 2025 - 16:06

Muhtasari


  • “Mwaka 2025 ni mwaka wa mwanamke kusugua goti, kwenda kwenye nyumba za ibada kwa ajili ya kuombea afya ya mume wako,” alimaliza 

Pasta akiomba mlimani//HISANI

MCHUNGAJI mmoja ameibua wasiwasi kwa wanandoa katika mitandao ya kijamii baada ya kufichua kile alichokiita kama utabiri wake kuhusu kitakachotokea katika ndoa nyingi mwezi Aprili.

Katika video hiyo ambayo imezua gumzo zikiwa zimesalia siku chache kukamilisha mwezi Machin a kukaribisha rasmi mwezi Aprili, mchungaji huyo alionekana akitoa utabiri bila kutetereka kwamba ndoa nyingi zitasambaratika sana mwezi huo wa 4.

Kwa mujibu wake, ndoa nyingi zitavunjika kwa sababu wanaume wengi watapoteza nguvu za kiume ghafla, huku wanawake wakilazimika kutafuta huduma kwa wanaume wengine wenye nguvu.

“Kuanzia mwezi wan ne 2025, wanaume nguvu za kiume zitapotea ghafla. Asilimia kubwa ya wanaume, nguvu za kiume zitakuwa zikipotea ghafla. Na ndoa nyingi sana zitaingia kwenye shida,” alihubiri huku waumini wakimtumbulia macho wasijue cha kufanya.

Kando na wanaume kupoteza nguvu za kiume ghafla, mchungaji huyo pia alisema hilo litawaweka wanawake walioko kwenye ndoa katika hatari ya kulazimika kuchepuka ili kutafuta kukidhi haja za miili yao.

“Wanawake wengi watatoka kwenye ndoa zao kwenda kutafuta wanaume wengine. Lakini yule mwanaume mpya atakayempata, baada ya kuwa naye kwa muda mfupi naye nguvu za kiume zitakuwa zimekata,” aliendeleza kupakua injili.

Alisema kwamba wanawake wengi kutokana na kutompata mwanaume mwenye nguvu za kiume kikidhi mahitaji yao ya tendo la ndoa, watakuwa wanazunguka kutoka kwa mwanamume mmoja kwenda kwa mwingine – yote hayo kuanzia Aprili mosi!

Kama ni kweli, basi ni mwaka ambao wanawake watakuwa wanawayawaya kama kuku aliyekatwa kichwa wakitafuta kukidhi mahitaji ya miili yao.

“Mwanamke huyo ataenda tena kwa mwanamume mwingine na kumkuta huyo pia nguvu za kiume hana. Ni mwaka ambao wanawake watakuwa wanawayawaya.”

Hata hivyo, mahubiri yake hayakukamilika bila kutoa suluhisho kwa utabiri huo, haswa akiwalenga wanawake.

“Aprili 2025 ukimuona mumeo hana nguvu za kiume, tulia hapo hapo. Hapo utakapotaka kukimbilia penyewe pia hazitakuwepo. Muombee mumeo!” pasta alishauri.

Alisema kwamba mwaka 2025 ni wa mwanamke kuchukua usukani wa kufanya toba ya maombi kwa ajili ya ustawi wa familia zao.

“Mwaka 2025 ni mwaka wa mwanamke kusugua goti, kwenda kwenye nyumba za ibada kwa ajili ya kuombea afya ya mume wako,” alimaliza waumini wakimpigia makofi.

Tazama video hiyo hapa;

 

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved