
MHUBIRI mashuhuri, kutoka Nigeria Mchungaji David Ibiyeomie anaamini kwamba Yesu hakuwahi kuwapenda maskini hata kidogo wakati wa enzi zake duniani.
Haya ni kulingana na klipu moja ya
mahubiri yake tata ambayo imekuwa ikikosolewa kwenye mitandao ya kijamii.
Mchungaji huyu katika klipu hiyo,
alidai kwamba Yesu wakati wa huduma yake ya miaka 33 duniani, hakuna hata siku
moja alimtembelea mtu maskini na kuingia katika nyumba yake.
Kasisi huyo alitoa marejeo ya kibiblia
ili kuendeleza hoja yake juu ya hili, kwani alitoa mifano ambapo Yesu
aliwatembelea matajiri pekee.
Mchungaji David Ibiyeomie alishikilia
kwamba Mkristo hapaswi kuwa na mawazo duni, kama Kristo tayari alikufa ili
kuhakikisha kwamba wao si maskini.
Aliwacha wakiristo changamoto ya kutoa
kifungu chochote kwenye Biblia kinachoesimulia au kumuonyesha Yesu akitembea na
kuingia katika nyumba ya maskini.
Alisema kwa sehemu…
"Yesu hakuwahi kumtembelea maskini
yeyote nyumbani, soma biblia yako. Maana yake anachukia umaskini.”
Mchungaji huyo alizama zaidi kutolea
mifano ya baadhi ya wahusika kwenye Biblia ambao Yesu aliwatembelea na kutoa
sababu zake kwa nini anaamini wahusika hao hawakuwa maskini.
“Cheki, alimtembelea Lazaro, hawakuwa masikini, walikuwa wakimpa chakula. Alimtembelea mwenye dhambi aitwaye Zakayo ambaye alikuwa tajiri; niambie yule maskini Yesu aliingia nyumbani kwake; anachukia umaskini maana yake, anachukia watu ambao ni maskini. Alikufa kwa ajili yako usiwe maskini wa akili ili uje kanisani. lakini huruhusiwi kubaki maskini…”
Mahubiri yake yalizua mchanganyiko
miongoni mwa waumini wa mitandaoni, baadhi wakimtaka kuelezea kifungu
kinachosema kwamba itawawia vigumu matajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni
kama ngamia kuingia kwenye tundu la sindano.
Wengine walimpinga kwa Kauli yake
kwamba Lazaro alikuwa tajiri wakisema kwamba alikuwa maskini wa kutupiwa
makombo ya chakula sakafuni.
Haya hapa ni baadhi ya maoni;
@Bobbydbobo aliandika: "Hawa
wachuuzi sha. Yesu sawa na kusema "Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita
katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu."
Watataka kuendeleza mazungumzo ya nyumbani juu ya ufanisi kwa faida yao wenyewe
na kisha kupotosha Biblia.”
@AtarodoScotch alisema: "Ikiwa hii
ni kweli. Kwa heshima zote 'Wewe ni Wazimu Bwana' kwa sababu Watin iwe hivi 😤🙄"
@VivienVivico aliandika: “Je, Lazaro
rafiki yake alikuwa tajiri? Je, mama-mkwe wa Petro alikuwa mwanamke tajiri?”