โข benbills007 alisema: "Hilo ni jambo moja kuhusu kamari ๐..Utashinda, lakini siku watakapoenda kukusanya pesa zako zote, utalia siku hiyo ๐."
Mwanamume mmoja mwenye umri wa makamo aliishiwa na nguvu na kupoteza fahamu kwa muda baada ya kupoteza laki mbili katika mchezo wa Kamari muda mfupi tu baada ya kushinda pesa hizo kutoka kwa mchezo huo huo wa Kamari.
Kwa mujibu wa blogu ya GossipMill iliyochapisha hadithi hiyo, mwanamume huyo alibahatika kushinda mchezo wa Kamari na kupata Naira laki mbili lakini tamaa ikamuingia na kupata msukumo wa kutaka kushinda Zaidi.
Hapo ndipo alianza na kuweka kima cha Naira elfu 40 ambazo zilienda na kabla hajagutuka, akapata laki mbili zote zimeshakunywa maji ndani ya muda mfupi tu, na furaha ikageuka kuwa majonzi.
Video iliyoenea kwenye mitandao ya kijamii ilinasa wakati wa kuhuzunisha kijana alijikuta kutokana na uwekezaji wake duni, na alionekana amejilaza kwenye godoro akiwa ameishiwa na nguvu huku akiwa hataki kabisa kuiona simu yake baada ya kupoteza mpunga.
Haya hapa ni baadhi ya maoni ya watu katika chapisho hilo;
benbills007 alisema: "Hilo ni jambo moja kuhusu kamari ๐..Utashinda, lakini siku watakapoenda kukusanya pesa zako zote, utalia siku hiyo ๐."
dansky_exchange alitoa maoni: โDau kamwe si njia ya kupata pesaโฆnyumba hakika itashindaโฆUTPOTEZA PESA YAKO.:
mcjblazedwfc alitoa maoni yake: "Tukikimbia Pesa sasa atakwenda bado kubeba Man U kushinda au sare ๐๐๐."
king_cozzy_ alibainisha: "Pesa atatumia kununua shuka mpya ๐๐๐๐."