Harmonize athibitisha mapenzi kwa mkewe wa Rwanda kwa njia ghali baada ya Kajala kumdhalilisha

Bosi huyo wa Kondegang aliweka wazi kuwa Phiona si mpenzi wake bali ni mke wake.

Muhtasari

•Harmonize alifichua kuwa amemnunulia mrembo huyo mwenye umbo wa kuvutia gari nyeupe aina ya Velar Range Rover.

•Mwimbaji huyo wa kibao 'Single Again' alidokeza kuwa anajivunia mwenyewe kwa kupata njia ya kupenda tena. 

amemthibitisha Phiona kama mpenzi wake mpya.
Harmonize amemthibitisha Phiona kama mpenzi wake mpya.
Image: HISANI

Staa wa Bongo, Rajab Abdul Kahali almaarufu Harmonize amethibitisha mapenzi yake mazito kwa mwanasosholaiti wa Rwanda Phiona almaarufu Yolo The Queen kwa njia ya kipekee na ya gharama kubwa.

Siku ya Jumanne, bosi huyo wa Konde Music Worldwide alifichua kuwa amemnunulia mrembo huyo mwenye umbo wa kuvutia gari nyeupe aina ya Velar Range Rover.

Konde Boy alichapisha video ya gari hilo la gharama alilomnunulia Phiona kwenye ukurasa wake wa Instagram na kubainisha kuwa kutumia pesa kwa ajili ya mtu anayempenda ni njia ya kuonyesha mapenzi yake kwake.

"Ninaposema nakupenda!!! Pesa zangu ni zako mwenyewe. Hongera sana boss @yolo_the_queen," Harmonize alisema kwenye Instagram.

Mwimbaji huyo wa kibao 'Single Again' alidokeza kuwa anajivunia mwenyewe kwa kupata njia ya kupenda tena. Pia alidokeza kwamba sasa tayari anaweza kuzungumza lugha ya Kinyarwanda kwa hisani ya mpenzi wake mpya.

Wakati akijibu moja ya blogu za Kenya, mwimbaji huyo wa zamani wa WCB aliweka wazi kuwa Phiona si mpenzi wake bali ni mke wake.

“Nyie acheni kusema kuwa nimemnunulia gari mpenzi wangu, bora niseme mke wangu maana tupo kwenye kiwango hicho,” alisema Harmonize.

Phiona anasemekana kuwa mmoja wa wanasosholaiti waliofanikiwa zaidi nchini Rwanda na vitongoji  vyake. Ameweza kunasa umakini wa watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii haswa wanaume, kwa hisani ya mwili wake wa kipekee uliopinda.

Mwanamitindo huyo mrembo na mshawishi wa Instagram anajulikana kwa misemo yake ya kuvutia 'Wake Pray Slay' na 'Sweeter than honey."

Wakati alipoulizwa kwa nini hapendi wanawake wenye makalio madogo na kupendelea wale wenye makubwa, Harmonize alisema, "usikutane naenda kuolewa, msichana wa namna hiyo!!! Inshallah juu ya Mungu, lakini kila mwanaume anapenda mwanamke. kwa kitako!! Wengine hawawezi kusema hata dada zetu wenyewe wanajua ukweli."

Staa huyo wa bongo fleva pia alikuwa na ujumbe kwa Watanzania wanaomkosoa kwa kutafuta mwanamke wa kigeni akidokeza kuwa tayari alishajaribu wa huko nyumbani lakini wakachukulia mapenzi yake kuwa ni mzaha tu.

"Kuna wadada nilikutana nao nikawaambia nakupenda, nichukue, tufanye hivi!!! Naweza kukufanyia hivi!! Walidhani natania. Leo ndio wanaanza kuleta uzalendo, sijui" najua taifa kwanza," alilalamika.

Harmonize alimtambulisha Phiona kama mpenzi wake mpya mwezi Mei lakini amekuwa kimya kumhusu katika kipindi cha miezi miwili iliyopita.

Thibitisho ya mapenzi yake kwa malkia wa Rwanda linakuja siku chache tu baada ya yeye na aliyekuwa mpenzi wake, muigizaji Kajala Masanja kushambuliana na kuaibishana hadharani kwenye mtandao wa Instagram.