Wimbo wa Bahati kwa Diana wafutwa You Tube

Serikali tusaidie kukabiliana na wezi hawa, hapa ndipo tunatoa ushuru wetu

Muhtasari

•, “Wapenzi mashabiki wa Bahati, Ziiki Media imeingia katika chanel yangu ya You Tube na bila idhini wakafutra wimbo wangu wa Diana nilohususisha Mrwanda Bruce Melodie, Ziiki Media ni wezi wa mitandao.”

Diana Marua kupewa zawadi ya siku ya kina baba na mumewe
Diana Marua kupewa zawadi ya siku ya kina baba na mumewe
Image: Instagram

Bahati ameeleza kusitikishwa na tukio  ambalo limemfanyikia katika chaneli yake ya You Tube.

Msanii huyo amekiri kwamba wezi wa mitandao wamepenya katika chaneli hiyo, na bila idhini wakaufuta wimbo ambao ameuweka muda mchache uliopita.

Katika ujumbe wake Bahati, alisema “  DEAR BAHATI FANS...ZIIKI MEDIA HAS ILLEGALLY HACKED MY YOU TUBE CHANNEL AND DELETED MY SONG DIANA FEATURING RWANDA’S BRUCE MELODIE...ZIIKI MEDIA ARE FRAUDSTERS” Kauli hiyo ambayo inatafsiriwa kuwa, “Wapenzi mashabiki wa Bahati, Ziiki Media imeingia katika chaneli yangu ya You Tube na bila idhini wakafuta wimbo wangu Diana, nilohususisha Mrwanda Bruce Melodie, Ziiki Media ni wezi wa mitandao.”

Katika ukurasa wake wa Instagram, Bahati aliomba msaada kwa serikali ya Kenya,akidai kwamba hapo ndipo wanatoa ushuru wao na akasihi kusaidiwa kukabiliana na wezi hao wa mitandaoni. 

Dear Kenyan Government this is Where we are getting our Taxes... Help Us Deal with this Fraudsters!!! VERY SAD!!” Aliposti baada ya kufahamu wimbo wake umefutwa. Ambayo katika tafsiri ni kuwa; “ Mpenzi Serikali ya Kenya, hata ndipo tupata Ushuru wetu...Tusaidie kukabiliana na wezi hawa! Yahuzunisha sana!

Wimbo uliofutwa msanii huyo alikuwa amekiri kuwa wa spesheli kwa mkewe Diana, baada ya zawadi walizopokezana na ambapo waliunda video alipokiri kuwa lazima wimbo huo angeuachilia saa saba mchana Juni 21.