Mnaweza nigusa popote bora msinishike sehemu za siri - Spice Diana kwa mashabiki

"Mashabiki wetu wanatupenda sana na wanapotuona kwenye jukwaa wanafurahi na kutaka kuhakikisha kama kweli ni sisi wale wanaoonekana kwenye runinga." alisema.

Muhtasari

• “Sitaki kuweka pengo lolote baina yangu na mashabiki wangu. Sioni sababu yoyote mbona wasiniguse" - Spice Diana.

• Diana alionekana katikati ya wahudhuriaji na alilalamika vikali kwa washereheshaji hao walioanza kumshika kwa njia isiyofaa miguuni.

Spice Diana asema haoni vibaya mashabiki kumgusa.
TAMASHA Spice Diana asema haoni vibaya mashabiki kumgusa.
Image: INSTAGRAM

Mwimbaji wa Uganda, Spice Diana jina halisi Hajarah Namukwaya ameweka wazi kuwa hana tatizo na mashabiki kumgusa wakati anatumbuiza kwenye shoo au tamasha la hadhara.

Mrembo huyo alifichua haya baada ya mashabiki kuonekana wakimgusa kwa njia isiyofaa wikendi iliyopita alipokuwa anatumbuiza kwenye tamasha moja kwenye wilaya ya Rukingiri.

Diana alionekana katikati ya wahudhuriaji na alilalamika vikali kwa washereheshaji hao walioanza kumshika kwa njia isiyofaa miguuni.

Spice Diana alilazimika kusitisha uchezaji wake na kuwaonya mashabiki dhidi ya kumgusa dhidi ya mapenzi yake lakini hii haikuwazuia mashabiki waliochangamka kuendelea.

Wakati akishiriki katika mahojiano mwishoni mwa juma, Spice Diana alipewa jukumu la kuzungumzia tabia mbaya inayoendelea miongoni mwa mashabiki ya kuwagusa wanamuziki isivyofaa.

Katika majibu yake, Spice Diana alifichua kuwa, tofauti na wanamuziki wenzake wengine, anapendelea kuigiza karibu na hadhira yake kwa sababu inamletea ubinafsi wake bora zaidi.

Alisema kwa sababu matendo yao yanachochewa na msisimko, yeye hana tatizo wafuasi wake wanapomgusa na kuingiliana naye wakati wa onyesho.

“Sitaki kuweka pengo lolote baina yangu na mashabiki wangu. Sioni sababu yoyote mbona wasiniguse, ilmradi wasiniguse kwenye sehemu zangu za siri na kwenye matiti. Mashabiki wetu wanatupenda sana na wanapotuona kwenye jukwaa wanafurahi na kutaka kuhakikisha kama kweli ni sisi wale wanaoonekana kwenye runinga. Wakati mwingine nawakaribia na kutaka kuwahisi pia,” Spice Diana alisema.

Spice alishikilia, hata hivyo, kwamba yeye huwa mwangalifu kila wakati mashabiki wanapomkaribia kwa sababu wanaweza kugusa sehemu zake za siri au sehemu nyingine nyeti za mwili.

Wikendi iliyopita Diamond Platnumz alionesha mapenzi yake makubwa kwa Diana akifichua kwamba walikuwa wanaandaa collabo yao kabla ya kuondoka kweney tamasha la Comedy Store.

Platnumz kwa maneno yake alisema kwamba Spice ni kama dadake na asingependa kumtafuna lakini pia akasema kuwa ikiwa lolote litatokea kati yao, hakuna atayelaumiwa kwani wao ni watu wazima.