Nashukuru Mungu niko hai-Bien asema baada ya kuhusika katika ajali

Mwimbaji huyo aliendelea kusimulia jinsi ajali hiyo ilivyotokea akifichua kuwa kulikuwa na athari kubwa kwa gari lake kufuatia ajali hiyo.

Muhtasari
  • Haijulikani mwimbaji huyo alikuwa akienda wapi na ajali hiyo ilitokea wapi lakini gari lake lilionekana kuharibika kutokana na picha aliyoshiriki.
Bien wa Sauti Sol.
Bien wa Sauti Sol.
Image: Screengrab

Mwimbaji Bien Aime Baraza amenusurika katika ajali ya barabarani.

Haijulikani mwimbaji huyo alikuwa akienda wapi na ajali hiyo ilitokea wapi lakini gari lake lilionekana kuharibika kutokana na picha aliyoshiriki.

Akitoa shukrani zake kwa kuwa hai, Bien aliandika kwenye ukurasa wake wa instagram na kusema;

"Asante Mungu nimetoka nikiwa hai."

Wiki iliyopita, mwimbaji mwenzake wa Kenya Nadia Mukami pia alisimulia jinsi alivyoponea kwenye ajali ya gari.

Katika taarifa ya video aliyotoa Jumapili jioni, mchumba huyo wa mwimbaji Arrow Bwoy alisema ana bahati ya kunusurika kwenye ajali hiyo aliyotaja kuwa shambulio la kiroho.

“Sijawahi kupitia tukio kama hilo. Ninamshukuru Mungu tu kwamba niko hai. Leo nahisi ni kama shambulio la kiroho, naapa kwa Mungu,” Nadia alisema.

Mwimbaji huyo aliendelea kusimulia jinsi ajali hiyo ilivyotokea akifichua kuwa kulikuwa na athari kubwa kwa gari lake kufuatia ajali hiyo.

“Tulipata ajali. Tulikuwa sehemu tofauti tukielekea upande mmoja na ajali ilitokea kwa wakati mmoja, ni mbaya kiasi gani. Sisi tuliponea. Ikiwa ingekuwa trela labda nisingekuwa hai. Nashukuru ilikuwa gari ndogo kwa sababu athari kwenye gari ni kubwa sana,” alisema.

Nadia alifichua kuwa licha ya yeye na wengine waliokuwa ndani ya gari ambalo alikuwemo kunusurika, dereva aliyekuwa kwenye gari hilo lingine aliachwa na majeraha mabaya sana.

"Yuko katika hali mbaya sana, hali mbaya sana. Siwezi hata kueleza hilo. Leo ilikuwa ya kutisha. Ajali zinatisha sana. Lakini namshukuru Mungu kwamba niko hai na niliweza kwenda nyumbani kwa mwanangu,” alisema.

Mama huyo wa mvulana mmoja alifichua kwamba alifika nyumbani usiku wa Jumapili kwani kwanza alipitia hospitali baada ya ajali hiyo.

"Nimekuwa hospitalini na yule jamaa mwingine. Jamaa huyo mwingine bado yuko hospitalini," alisema.