Wanawe Diamond wazidiwa na hisia baada ya kumtembelea wamuacha Diamonda na huzuni

Katika klipu ya video iliyochapishwa kwenye Insta Diamond anaonekana akiwa na wakati mzuri n wanawe pamoja

Muhtasari

β€’ Mwimbaji huyo anayetokea  Tanzania alisafiri kwa ndege hadi Afrika Kusini ili kutumia wakati mzuri na binti yake Tiffah na mwanawe Nillan.

β€’ Katika klipu ya video iliyochapishwa kwenye Insta Diamond anaonekana akiwa na wakati mzuri n wanawe pamoja. 

Diamond Platnumz/Instagram
Diamond Platnumz/Instagram

Msanii Diamond Platnumz aliumia sana moyoni kuona watoto wake wawili wakimlilia sana wakati alipokuwa anawaaga.

Mwimbaji huyo wa bongo alisafiri kwa ndege hadi Afrika Kusini ili kutumia wakati mzuri na binti yake Tiffah na mwanawe Nillan.

Akiwa nchini Sudan Kusini, Diamond alisisitiza mapenzi yake kwa Tiffah ambaye bila shaka ndiye mtoto anayependelea kuwa kipenzi chake.

Katika klipu ya video iliyoweka kwenye Insta Diamond anaonekana akiwa na wakati mzuri na wanawe pamoja. 

Hata hivyo alishindwa kubaini lengo la wanawe wakati wakimzuia kuondoka kwenda kufanya shughuli zake.

"Jamani,mpaka nimelia mwenzenu. Hawa watoto lengo lao ni nini kulilia baba yao alale kwao,ila wamenoga," alichapisha Juma Lokole kwenye video hiyo.

Agosti mwaka jana, Diamond alifichua kuwa alimchagua Tiffah kurithi sehemu kubwa ya utajiri wake.

Akizungumza katika mahojiano na kituo kimoja cha redio cha Afrika Kusini, msanii huyo wa Bongo  alisema kuwa anataka Tiffah asimamie himaya yake kubwa ya biashara.

"Ningependa yeye (Tiffah) awe mrithi wa mali yangu. Hasa biashara yangu ya muziki, niweze kusimamia biashara zangu. Hicho ndicho ninachotaka," Diamond alisema.

Mwimbaji huyo wa Tanzania alikariri zaidi kuwa hataki binti yake awe mwanamuziki kama yeye.

β€œSitaki ateseke. Nisingependa apitie mateso ambayo nimepitia. Nataka awe mrithi wa biashara nyingi ambazo pia nimemwanzishia,” alisema.

Kurudi Oktoba 2023, Diamond alikuwa na wakati mgumu alipokuwa akiwaaga watoto wake wawili kwaheri.

Wote Tiffah na Nillan waliangua kilio huku wakimuona baba yao akiondoka kuelekea Tanzania jamb ambalo pia lilimuacha Diamond akiwa na huzuni mwingi kuona jinsi wanawe walivyomwaga machozi.