Watu Wawili Wajeruhiwa Baada Ya Ndege Kuanguka Taita Taveta

Watu wawili wanatibiwa katika hospitali ya Wesu huko Wundanyi kaunti ya Taita Taveta wakiwa na majeraha mabaya baada ya ndege walimokuwa wamesafiria kuanguka katika eneo la Kungu.

OCPD wa Mwatate amethibitisha kisa hicho japo haijabainika ndege hiyo ilikokuwa ikielekea. Amesema ndege hiyo inamilikiwa na serikali.
-Solomon Muingi