Jamaa amuua mkewe na kisha kujitia kitanzi

Mwanamume mmoja katika Kaunti ya Kakamega amemuua mkewe na kisha kujitia kitanzi.

Kisa hicho kilitokea katika mtaa wa Mawe Tatu eneo bunge la Likuyani.

Wawili hao inasemana walikuwa wamezona kuhusiana na changamoto katika ndoa yao. Miili yao iligunduliwa na majirani asubuhi ya Jumanne.

Kwingineko, wasimamizi wa hospitali katika kaunti ya Kakamega wemonywa dhidi ya kuendelea kuwatoza ada wanachama wa bima ya NHIF.

Afisa NHIF katika kaunti hiyo Benard Kirui anasema wamegundua kuwa baadhi ya hospitali katika kaunti hiyo zimekuwa zikikiuka makubaliano kati yazo na NHIF kwa kuwatoza wanachama wa bima hiyo.

Anasema wale watakaopatikana watasakwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

NA CYRUS AKHONYA